
Ikulu Zanzibar
50.6K subscribers
Verified ChannelAbout Ikulu Zanzibar
Chaneli rasmi ya habari za Ofisi ya Rais Ikulu Zanzibar
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

RAIS MWINYI:SMZ ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA VODACOM TZ. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kushirikiana na Kampuni ya Vodacom Tanzania katika kuharakisha huduma za kidigitali nchini. Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo alipokutana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire na ujumbe wake Ikulu Zanzibar tarehe 1 Machi 2025. Naye , Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania Philip Besiimire ameeleza kuwa Vodacom itapanua huduma zake Zanzibar kwa ajili ya uwekaji wa huduma za kidigitali katika sekta muhimu ikiwemo elimu, afya, na maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Halikadhalika, Besiimire amesema Vodacom Tanzania kupitia Foundation yake itajitolea kuboresha zaidi miundombinu ya kujifunza kielektroniki na kuwawezesha vijana na wanawake kwa ujuzi wa kidijitali na kifedha ikiwemo pia kuunganisha zaidi ya shule 100 Zanzibar ifikapo 2026.

RAIS MWINYI:ZNZ ITAONGEZA IDADI YA WATALII KUTOKA ASIA Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema Zanzibar inafanya kila juhudi kuhakikisha inaongeza idadi ya Watalii kutoka Barani Asia . Dkt.Mwinyi amesema hayo alipozungumza na Waigizaji na Watengenezaji wa Filamu kutoka India Waliofika Ikulu Zanzibar tarehe 1 Machi 2025. Aidha Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa Zanzibar iko tayari kushirikiana na India kutangaza Vivutio vya Utalii nchini humo na kuwataka kuwa Mabalozi Wazuri watakapokuwa nchini kwao. Halikadhalika, Rais Dkt.Mwinyi amesema Uzoefu na Umahiri wa Waigizaji na Watengezaji wa Filamu wa India ni fursa Muhimu inayoweza kutumika kuitangaza Zanzibar ili Kuongeza Watalii kutoka India. Vilevile Rais Dkt.Mwinyi amewapongeza kwa kuja nchini na Serikali ipo tayari kushirikiana nao kikamilifu kuitangaza Sekta ya Utalii ya Zanzibar. Naye Mkuu wa timu hiyo ya Waigizaji kutoka Taasisi ya JIO CREATIVE LABS Aditya Bhat amesema ziara yao imefungua fursa za Ushirikiano na wako tayari kuvitangaza Vivutio vyà Utalii vya Zanzibar nchini India kupitia fani zao.