
Abuu Mus'ab Media
1.6K subscribers
About Abuu Mus'ab Media
Graphics Designer
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

*HUKMU YA KUFUNGA BAADA YA NUSU YA SHA'BAAN* _"Ama kilichokuja kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وسلم - kutoka kwa hadith ya Abu Hureira رضي الله عنه kuwa alisema: *(itakapofika nusu ya Sha'baan msifunge)* ameipokea Abu Daud na Tirmidhi._ _*Ulamaa wamekhtalifiana katika kuisahihisha na kuidhoofisha, wameidhoofisha wengi katika ulamaa wa hadith, kama Ahmad na ibn Ma'iin, na hata kwa kauli kuwa ni sahihi kama walivyoenda kwa kauli hiyo ibnul Qayyim na Al Albani, na ibn Baz -Allah awarehemu wote; linalokusudiwa ni katazo la kuanza kufunga baada ya nusu ya Sha'baan, ama aliyekuwa amefunga masiku mengi ya mwezi basi amepata Sunnah.*_ _Asema Sheikh Ibn Utheymiin رحمه الله تعالى -: *"na hata lau hadithi itasihi, basi katazo humo si ya kuharamisha, ni ya karaha (umakruhu) tu, kama walivyochukua kauli hiyo baadhi ya ahlul ilm, ila aliyekuwa na ada ya kufunga, basi atafunga hata baada ya nusu ya Sha'baan".*_ 📗[Khutba: Ahkaamu shahri sha'baan; ya Sheikh Khalid Adh-dhafiry-Allah amhifadhi] ════ ❁✿❁ ════ *Salafi Da'wah East Africa (Salafi Da'wah Afrika Mashariki)* https://whatsapp.com/channel/0029VabMSx07tkj3R6Dou41f

*🚫BIDA' KATIKA USIKU WA NUSU YA SHA'BAAN* *_Miongoni mwa yanayotakikana kutanabahisha juu yake katika yatakayokuja katika nusu ya huu mwezi (wa Sha'baan ) ni mambo waliyoyazua watu.._* *_Na miongoni mwayo ni:_* *_1-baadhi ya watu kukhusisha usiku wa nusu ya Sha'baan kwa swala au kusimama usiku pasi na masiku mengine, na kuhuyisha usiku huo kwa dhikr na dua na kusoma Qur'ani, basi hili ni bid'a katika dini upotofu, hakulifanya Mtume صلى الله عليه وسلم wala maswahaba wake, na hiki kitendo ni chenye kurejeshwa kwa mwenyewe (aliyetenda), Allah عز وجل haikubali._* *_2-kuusherekea usiku huu, na kuwakunjulia familia katika chakula na vinywaji na mavazi, na mfano wa hayo, na kuukhusisha usiku huo pekee kati ya masiku kwa kuitakidi ubora wake, na kuwa ni bora kuliko masiku mengine , na hili ni katika jambo ambalo halikuja katika sheria kulifanya, wala hakulipendekeza yeyote miongoni mwa maswahaba wala tab'iin رحمهم الله, na kisichokuwa dini wakati huo hakitakuwa dini leo._* 📗[Khutba: Ahkaamu shahri sha'baan; ya Sheikh Khalid Adh-dhafiry-Allah amhifadhi] ════ ❁✿❁ ════ *Salafi Da'wah East Africa (Salafi Da'wah Afrika Mashariki)* https://whatsapp.com/channel/0029VabMSx07tkj3R6Dou41f

*SIKU : IJUMAA* *TAREHE:* *7 FEBRUARI 2025 M* *8 SHA'BAAN 1446 H* *NASAHA ZA LEO: HII NDIYO HANIFIYYAH (MILA YA IBRAHIIM)* *SHEIKH : ABUU AYMAN ASHIRAZIY (ALLAH AMHIFADHI)* ©️MASJID IRSHAAD - ILALA DSM