Find WhatsApp Channels
Discover the best WhatsApp channels for news, entertainment, education and more. Our powerful search helps you find exactly what you're looking for.
Channels & Posts for #farnboroughinternationalairshow
Posts
Aviation Tanzania on Instagram: "Qatar Airways yatupilia mbali agizo la ndege 25 za Boeing 737 MAX 10. Shirika la ndege la Qatar Airways limethibitisha kusitisha mpango wake wa kununua ndege 25 aina ya Boeing 737 MAX 10, uamuzi ambao unatamatisha rasmi agizo hilo lililotolewa mwaka 2022 katika Maonyesho ya Anga ya Farnborough. Katika mahojiano na chombo cha habari cha Bloomberg, Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo, Badr Al-Meer, alifichua hatua hiyo, akiielezea kuwa ni sehemu ya mabadiliko ya mikakati ya shirika hilo katika usafiri wa ndani na wa masafa mafupi. Uamuzi huu umekuja wakati Qatar Airways ikiwa tayari imesaini agizo jipya la ndege zenye thamani ya dola bilioni 96 za Kimarekani kwa ndege 160 aina ya Boeing 787 na 777X, lakini imeamua kuachana kabisa na ndege za Boeing MAX 10. Mpango wa kufuta agizo hilo ulianza kuvuma Disemba mwaka jana, huku vyanzo vya habari vikidokeza kuwa MAX 10 haikidhi tena mahitaji ya sasa ya mtandao wa ndege za Qatar Airways. Ilitarajiwa kuwa shirika hilo huenda lingebadilisha agizo hilo na kuagiza Boeing 737 MAX 8, lakini hatimaye likachagua kufuta agizo lote. Agizo hilo lilitangazwa kwenye maonyesho ya Farnborough mwaka 2022 na aliyekuwa Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Boeing Commercial Airplanes, Stan Deal, ambaye aliitaja MAX 10 kama chaguo bora kwa mtandao wa safari za kikanda za Qatar Airways. Kwa sasa, Qatar Airways inaelekeza mikakati yake katika safari za masafa mafupi kwa kuagiza ndege kutoka kampuni ya Airbus. Kwa mujibu wa takwimu za ch-aviation, shirika hilo lina ndege 50 aina ya Airbus A321neo ambazo bado hazijakabidhiwa. #fleetexpansion #airline #qatarairways #boeing737max10 #airbus #farnboroughinternationalairshow #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"
https://www.instagram.com/p/DKHgrO4MvtT/?igsh=MXRmdHg1bnJlNWNnOQ== *Qatar Airways yatupilia mbali a...