Find WhatsApp Channels

Discover the best WhatsApp channels for news, entertainment, education and more. Our powerful search helps you find exactly what you're looking for.

Channels & Posts for #qatarairways

Posts

Qatar Airways: Flight Attendant Learnerships 2025 / 2026 | GILE JoBs | South Africa

Apply for Qatar Airways’ Flight Attendant Learnerships for the 2025 / 2026 academic year! For more ...

Aviation Tanzania on Instagram: "Qatar Airways yatupilia mbali agizo la ndege 25 za Boeing 737 MAX 10. Shirika la ndege la Qatar Airways limethibitisha kusitisha mpango wake wa kununua ndege 25 aina ya Boeing 737 MAX 10, uamuzi ambao unatamatisha rasmi agizo hilo lililotolewa mwaka 2022 katika Maonyesho ya Anga ya Farnborough. Katika mahojiano na chombo cha habari cha Bloomberg, Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo, Badr Al-Meer, alifichua hatua hiyo, akiielezea kuwa ni sehemu ya mabadiliko ya mikakati ya shirika hilo katika usafiri wa ndani na wa masafa mafupi. Uamuzi huu umekuja wakati Qatar Airways ikiwa tayari imesaini agizo jipya la ndege zenye thamani ya dola bilioni 96 za Kimarekani kwa ndege 160 aina ya Boeing 787 na 777X, lakini imeamua kuachana kabisa na ndege za Boeing MAX 10. Mpango wa kufuta agizo hilo ulianza kuvuma Disemba mwaka jana, huku vyanzo vya habari vikidokeza kuwa MAX 10 haikidhi tena mahitaji ya sasa ya mtandao wa ndege za Qatar Airways. Ilitarajiwa kuwa shirika hilo huenda lingebadilisha agizo hilo na kuagiza Boeing 737 MAX 8, lakini hatimaye likachagua kufuta agizo lote. Agizo hilo lilitangazwa kwenye maonyesho ya Farnborough mwaka 2022 na aliyekuwa Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Boeing Commercial Airplanes, Stan Deal, ambaye aliitaja MAX 10 kama chaguo bora kwa mtandao wa safari za kikanda za Qatar Airways. Kwa sasa, Qatar Airways inaelekeza mikakati yake katika safari za masafa mafupi kwa kuagiza ndege kutoka kampuni ya Airbus. Kwa mujibu wa takwimu za ch-aviation, shirika hilo lina ndege 50 aina ya Airbus A321neo ambazo bado hazijakabidhiwa. #fleetexpansion #airline #qatarairways #boeing737max10 #airbus #farnboroughinternationalairshow #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/p/DKHgrO4MvtT/?igsh=MXRmdHg1bnJlNWNnOQ== *Qatar Airways yatupilia mbali a...

Aviation Tanzania on Instagram: "Wanandoa wadai kulazimishwa kukaa pembeni ya mwili wa marehemu kwa masaa manne ndani ya ndege. Wanandoa wawili, Mitchell Ring na Jennifer Colin wamedai kuwa walilazimishwa kukaa kwa masaa manne pembeni ya mwili wa mwanamke aliyefariki kwenye ndege ya Qatar Airways iliyokuwa ikisafiri kutoka Australia hadi Qatar. Wanandoa hao walikuwa wakitokea Melbourne kuelekea Doha, mji mkuu wa Qatar, wiki iliyopita, masaa kumi baada ya ndege hiyo kuanza safari, mwanamke mmoja alitoka ndani ya choo na kuanguka kisha kupoteza maisha mbele yao. Wawili hao walieleza kwenye kipindi cha habari cha Australia “A Current Affair” siku ya Jumapili kuwa walifanya kila jitihada kuokoa maisha ya mwanamke yule, lakini ilishindikana, jambo ambalo lilikuwa gumu kutazama, alisema Ring. Ring alisema wafanyakazi wa ndege waliuweka mwili wa mwanamke huyo kwenye kiti kilichokuwa wazi karibu nao kwa masaa manne yaliyosalia ya safari yao. Walieleza kuwa,Bi.Jeniffer alikuwa pembeni ya mumewe Ring, wakiwa kwenye mstari wa viti vinne wahudumu walimwambia Jennifer ahamie upande wa pili wa mumewe naye alikubali bila shida, kisha wakauweka mwili wa mwanamke huyo kwenye kiti alichokuwa amekaa Jennifer mwanzoni. Wanandoa hao walisema wafanyakazi wa ndege hawakuwaruhusu kubadilisha viti kwa kipindi chote cha safari na waliwaomba wabaki kwenye viti walivyokuwa hadi wahudumu wa matibabu walipowasili. Qatar Airways, ambayo inamilikiwa na serikali ya Qatar, ilitoa taarifa siku ya Jumatatu ikitoa pole kwa familia ya abiria ambaye alifariki ndani ya ndege yao kwa bahati mbaya. Waliomba msamaha kwa usumbufu wowote uliojitokeza katika tukio hilo, na walikuwa kwenye mchakato wa kuwasiliana na abiria kulingana na sera na taratibu zao. . Chanzo-NBC News #qatarairways #deathonboard #aviationtanzania✈️ #AviationTanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzania✈ #aviatamedia"

https://www.instagram.com/p/DGiE2VutzUF/?igsh=NmRhc29sdmxlZDB6 *Wanandoa wadai kulazimishwa kukaa p...