
SAHIHI TV
February 10, 2025 at 06:46 AM
Wanajeshi wa Israeli wamejiondoa kutoka ukanda wa Netzarim - eneo la jeshi la kaskazini mwa Ukanda wa Gaza kutoka kusini.
#keyter
Mamia ya Wapalestina walionekana kwenye magari na mikokoteni iliyojaa magodoro na bidhaa zingine wakiwa wanarudi Kaskazini mwa Gaza kufuatia kujiondoa kwa vikosi vya Israeli – hasa katika maeneo yaliyoharibiwa zaidi.
Uondoaji wa vikosi vya Israeli unaambatana na makubaliano ya kukomesha mapigano ya Israeli-Hamas ya Januari 19 ambapo mateka 16 wa Israeli na wafungwa 566 wa Palestina wameachiliwa.
Mwisho wa hatua ya kwanza ya kusitisha mapigano katika muda wa wiki tatu, mateka 33 na wafungwa 1,900 wanatarajiwa kuachiliwa.
Israeli inasema nane kati ya 33 wamefariki dunia.