
SAHIHI TV
February 20, 2025 at 12:50 PM
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imeomba msaada wa kijeshi kutoka Chad ili kupambana na waasi wa M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda.
Kwa mujibu wa afisa wa Chad na chanzo ndani ya Ikulu ya Congo, Waziri wa Uhusiano wa Kanda wa DRC alikutana na Rais wa Chad, Mahamat Idriss Deby Itno, na kufikisha ombi hilo kwa niaba ya Rais Felix Tshisekedi.
#keyter