SAHIHI TV
SAHIHI TV
February 27, 2025 at 06:16 AM
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky atakutana na Rais wa Marekani Donald Trump mjini Washington Ijumaa ili kutia saini makubaliano ya kugawana rasilimali za madini za nchi yake, Trump amesema. Zelensky ameelezea makubaliano hayo ya nchi mbili kama ya awali, na akasema anataka makubaliano zaidi ambayo ni pamoja na dhamana ya usalama ya Amerika ili kuzuia uchokozi mpya wa Urusi. Lakini Trump alisema Marekani haitatoa hakikisho "zaidi ya ... sana", akisema jukumu hilo linapaswa kuwa la Ulaya. Trump pia inaonekana aliondoa uwezekano wa Ukraine kuwa mwanachama wa Nato - moja ya matarajio ya muda mrefu ya Zelensky. Akizungumza katika mkutano wa baraza lake la mawaziri siku ya Jumatano, Trump alisema kuwepo kwa wafanyakazi wa Marekani wanaochimba madini adimu kwenye udongo wa Ukraine kutatoa "usalama moja kwa moja" kwa Ukraine. Alisema Kyiv inapaswa "kusahau" kujiunga na Nato na kurudia madai ya Urusi kwamba suala hilo ni moja ya sababu zilizosababisha vita. Rais wa Marekani alisema kuwa usitishaji mapigano kati ya Ukraine na Urusi hauko mbali, akiwaambia waandishi wa habari kuwa: "Tutafanya makubaliano na Urusi na Ukraine ili kukomesha mauaji ya watu. Lakini Zelensky alisema bila hakikisho la usalama "hatutakuwa na usitishaji mapigano, hakuna kitakachofanyika, hakuna". "Nataka kupata njia ya Nato au kitu kinachofanana kama hicho," alisema. #keyter

Comments