UFUNDI KITANDANI❤️👙😍
UFUNDI KITANDANI❤️👙😍
February 11, 2025 at 09:08 PM
KUMBE WACHAWI NAO WATAMU 🔞🔞 SEHEMU YA 08 had 09 Vero akamtazama mwenzake akatabasamu na kuuliza “Ina maana umeshaamua kumfanya wa kwako??” “Ndio ni wa kwangu....wewe kilichokupeleka nini?” aliuliza kwa hasira Vero akasema “Kwa taarifa yako, mimi ndiye nilianza kutoka naye kwa hiyo usinisumbue, nitaenda nikitaka na nikiamua ninamloga anakuwa wa kwangu milele” alipomaliza sentensi hii Vero huyo akatoweka zake akiwa na speed ya kufa mtu. Hakukuwa na namna, tayari chuki ya mapenzi kati ya wawili hao ilikuwa imeshapanda, kila mmoja alikuwa ameelewa show aliyokuwa ameipata kutoka kwa kijana Hamis Kapweto. Hata hivyo kulikucha, jua likaanza kuwaka, lakini Changa alikuwa ni binti mstaarabu kidogo, alikuwa hajafuliwa kisawasawa kwenye uchawi, bado ubinadamu ulikuwepo. Aliondoka zake na kwenda moja kwa moja mpaka kwa Bi Mpwele, nia yake alitaka kwenda kujua anaendeleaje baada ya kukutana na maswahibu yote ya usiku, licha ya wachawi kutokufahamu chanzo kizima cha kiongozi wao kufika akiwa amepigika sana. Changa alibisha hodi, wajukuu wa bi Mpwele wakamkaribisha, “Nimemkuta bibi yenu??” aliuliza “Yupo ndani amelala anaumwa” alijibu mjukuu mmoja kati ya walr wawili waliokuwa wakichezea matope pale nje “Naweza kumuona” “Ndio, ingia ndani” alisema “Sawa” Changa aliingia katika chumba alichokuwa akilala bi Mpwele na alipofika kule alimkuta bi Mpwele akiwa amelala chali anatokwa na machozi, mwili unamuuma kila mahali. “Bibi” aliita Changa akiwa anaketi kwenye kitanda kando ya bi Mpwele Bi Mpwele alinyanyua macho na kutazama akagundua ni Changa, akamuuliza “Mbona nimekuita sana lakini umechelewa kufika Changa??” aliuliza “Umeniita saa ngapi?” “Nimekuita kwa kukutumia Jini lakini hujaitika” “Oh mtambo haufanyi kazi, damu yote tulikumiminia jana nimebaki sina mafuta bibi” “Sawa....ni kheri umekuja mwanangu....ninaumwa sana” Changa alimsogelea na kumuuliza kwa mnong’ono “Kwani ulipatwa na nini bibi?” Bibi Mpwele akasema “Nikuambie kitu kimoja, kama nitakuwa hai au nimekufa, tujihadhari sana na uchawi wa Bi Kamlenga, ni hatari, amenipiga kama mtoto jana nilienda kujaribu kumshambulia” “Kwanini ulienda na unajua ni hatari bibi yule??” aliuliza Changa “Nisingeweza kuacha kwa sababu amenitishia mara nyingi sana, nimetumia nguvu zangu zote lakini aliponigusa na ncha ya kidole mkono ulikuwa kama umepooza” “Ohooo....leo utafika kweli?” aliuliza Changa “Ni ngumu kuja kwa sababu fisi wangu alimdanganya na kumteka amemuiba ameshakuwa wake” “Kweli??” aliuliza “Ndio ni wake, naomba uende kwa Sophia muambie awashe mtambo, yeye atasimama kama kiongozi wenu mpaka nitakapokuwa sawa” “Sawa nitafanya hivyo” alisema Changa “Sasa hivi” alisisitiza bi Mpwele Changa aliondoka pale kwa bi Mpwele, kichwani alijiuliza mwaswali mengi sana, mara zote kilichokuwa kikimjia akilini ni suala zima la bi Kamlenga, binti alijiuliza sana kwamba bi Kamlenga ni nani mbona ana nguvu kubwa ya uchawi kiasi cha kumdhuru hata kiongozi wao. Mwanzo Changa aliamini kwamba hakuna mtu yeyote mwenye uwezo wa kumtishia bibi Mpwele kwa sababu alikuwa anaziaminia kazi zake kwa kiasi kikubwa sana, ndiye aliyemfundisha uchawi baada ya kumteka binti akiwa anasoma shule ya sekondari, lakini Changa alikolea katika uchawi kuliko kawaida na kutokutaka kuchomoka humo kabisa. Siku ile Changa alitamani sana kumfahamu huyo bibi Kamlenga ambaye amekuwa tishio kwa ngome zingine za kichawi, lakini pia hakufahamu kwamba bibi Kamlenga mwenyewe ni bibi yake mwanaume ambaye alikuwa na sukari yake, ambaye nia Hamis Kapweto. Changa alienda mpaka kwa Bi Sophia akamueleza awashe mtambo kiongozi anataka kuwasiliana naye, lakini pia Changa alimuomba kitu kimoja kwamba usiku ampangie mtaa wa kagera ili aweze kwenda kumfaidi Kapweto. Bi Sophia alikubali lakini changa alikumbuka kwamba usiku uliopita alikuwa amempiga Kapweto, hivyo binti akaanza kuogopa na kuamua kwenda mpaka pale kwenye biashara za yule kijana ili aweze kumuomba msamaha......JE KAPWETO ATAMSAMEHE?? USIKOSE SEHEMU YA 09 Kabla ya binti Changa kuanza safari yake ya kwenda moja kwa moja kwa Kapweto ili amuombe msamaha, aliona ni heri akajiandaa avae vizuri kisha aende ili aweze kuwa na mvuto wa aina yake. Alikuwa mwenye umri wa miaka 19 tu lakini alijua kupangilia mavazi, mtu akimuangalia kwa jinsi alivyokuwa mzuri, kamwe asingeweza kuamini yule binti ni bonge la mchawi, mwenye nguvu nyingi za kuogopesha. Changa alivaa nguo ndefu sana, kisha akachana nywele zake na kuzilaza nyuma, zilikuwa sio ndefu sana lakini zilikuwa laini maana alipenda kuzitunza, alijifunika na mtandio mweupe kichwani halafu akavaa viatu vya wazi na safari ilianza kuelekea mtaa wa Kagera Alitembea taratiibu, lakini vile vile aliogopa maana tayari alikuwa ameshampenda mwanaume ambaye alienda kumuwangia usiku. Alipofika karibu na pale alipokuwa akiishi Rasi Kapweto, binti alitazama kwa makini akagundua kuna wazee wengi sana wanapata vileo muda ule. Ikabidi asite na kuwaza namna ya kumuendea. Akiwa anawaza ataendaje pale, ndipo alipopata wazo la kumuagiza mtu yeyote ambaye alikuwa anapita pale, hata hivyo haikuchukua muda mrefu sana, alipita mwanamke mmoja ambaye alikuwa akiitwa mama Asha. Bila shaka mama Asha alikuwa ni mteja mzuri wa Hamis Kapweto na siku mbili kabla ya ile alikuwa amemuambia Hamis aachane na huyo mtoto maana ni mwanga na amevunja ndoa nyingi sana. Binti bila kujua yule mama anamfahamu vizuri, alimuita “Samahani mama” alisema na mama yule aligeuka akakuta ni Changa, akashtuka na kusema “Bila samahani” alisema mama Asha “Shikamoo kwanza” alisema Changa “Marahaba” “Ah..mh unaelekea hapo kwa rasi??” “Ndio” “Basi naomba unisaidie kumuita mwambie niko hapa” Mama Asha alimtazama juu mpaka chini, akakumbuka juzi tu alikuwa ameshampa onyo, ndipo akasema “Haya nitamuambia” “Sawa asante” Mama Asha aliendelea na safari yake mpaka akafika kwa rasi, ambapo alikuta watu wengi na aliwasalimia halafu akamfuata rasi na kumuambia “Hamis, una mgeni wako kule” Hamis Kapweto akashtuka na kuinuka akatazama, ni mbali kidogo na pale hivyo hakufanikiwa kujua ni nani, zaidi alijua ni mwanamke ambaye amevaa nguo nyeupe. “Ni nani huyo??” aliuliza rasi “Ni yule binti ambaye nilikupa onyo juzi, naona kaamua kukufuata mpaka huku” Hamis alishtuka sana baada ya kusikia vile, akajiuliza kwanini yule binti alikuwa anajipendekeza kwa kiasi kile, ndipo akamuhudumia mama Asha halafu akamfuata Changa. Alipofika kwa Changa alimkuta Changa akiwa anatabasamu tayari. Changa akamuamkia “Shikamoo kaka rasi” Hamis Kapweto hakujibu salamu, ila alimuuliza “wewe ndiye umeniita??” “Ndio…nimeona watu wengi sana pale, nikaogopa kukufuata” “Pole sana” alisema “Hivi nikuulize kwanza hivi jina lako halisi unaitwa nani??” Changa akatabasamu na kujibu “Naitwa Changa” “Nini? Shanga??” Changa akacheka na kujibu “Sio shanga, ni Changa bhana” alisema “Ahaaa…nina wateja niambie ulichoniitia” “Ah nimekuja kukuomba msamaha kwa kile nilichokufanyia usiku” alisema “Kwani ulifanyeje??” “Naamini nilikuumiza nilipokukuta ukiwa na mwenzangu……” “Ah usijali” alijibu rasi “Basi mi naondoka” “Hapana usiondoke kwanz…..ninahitaji kitu kutoka kwako” alisema “Kitu gani” “Kaka Hamis naomba niwe mpenzi wako” alisema “Khee tena?” aliuliza “Ndio, mwenzako mi nimekupenda nimenogewa na penzi lako…..” Hamis alimtazama Changa kuanzia juu mpaka chini kweli ni binti mzuri, halafu hata hatumii gharama, kila siku ni kupewa tu, binti akasema “Ila nataka niwe peke yangu usiwale wale wengine” “Duuh….usiku unakuja?” aliuliza Kapweto “Yes nitakuja” “Okay tutaongea zaidi, ngoja niende kule wasije wakaniibia” “Sawa ila” “Ila nini??” “Naomba namba yako” alisema Changa huku akiitoa lock simu yake “Okay…..07……………….” Changa aliiandika kisha akaondoka zake. Binti aliondoka akarudi nyumbani akiwa na furaha tele, kiukweli hata Rasi mwenye alikuwa ameshamzimia mtoto Changa, alikuwa na penzi tamu, alikuwa fundi kushinda hata Vero, halafu ndo kabisa ni katoto, kuwa na katoto nako kuna raha yake. Hamis aliendelea na majukumu yake ya kila siku Sasa wakati Changa anarudi nyumbani, ndipo njiani akakutana na Vero, tena alikuwa amebeba kuku mweusi na anaelekea kule kule kagera kwa rasi. Changa akashtuka na kumuuliza “Unampeleka wapi kuku wako huyo?” aliuliza Changa huku akionyesha dhahiri kutokufurahishwa na kitendo hicho “Embu pita zako, kwani yanakuhusu nini??” alisema Vero na kumpita akaendelea na safari JE VERO ANAPELEKA WAPI KUKU MWEUSI?? USIKOSEEEE SEHEMU YA 10
👍 🙏 2

Comments