UFUNDI KITANDANI❤️👙😍
UFUNDI KITANDANI❤️👙😍
May 25, 2025 at 10:53 PM
`JINSI MWANAMKE NAVYO GEUKA KUA KERO KWA MWANAUME.`📚🥰📚 ✍️..Mwanzo ya uchumba hukua na wasiwasi wowote, wakati unaanza naye mahusiano ulikua unajua unapita tu hivyo hukuwa unajali sana. Huenda Yeye ndiyo alikua anapiga simu mara kwa mara, anatuma meseji na kila kitu anafanya yeye. Lakini sasa hivi baada ya ndoa kila kitu kimebadilika, akiwa mbali unatamani kuongea naye, ukimuona online unatamani kumtumia meseji hata mchart, Kama alizoea kukupigia simu mara tatu sasa hivi anapinga moja mwili unawake moto, unahisi kama kashaanza kukuchoka , au kama kuna kitu kibaya kinaendelea. Kuna wanaume wanapenda hii hali, lakini sasa kama wakwako anakasirika basi soma hapa; (1) Jinsi uanvyozidi kumzoea mwanaume ndiyo jinsi uoga wa kumpoteza unaongezeka, mawazo hasi ya kumpoteza yanakutawala, Unahisi kabadilika, hakupendi tena, hafurahii kuongea na wewe, kuna mtu ana umuuhimu kwake kuliko wewe. Sasa kinachotokea hapa nikuwa, kwakua una mawazo hasi sana, badala ya kufurahia ndoa yako unakua na wasiwasi, huna furaha, visirani vinakua vingi, unahisi anakufanyia mambo mabaya hivyo unakua huna amani. (2) Kwakua unaogopa kumpoteza basi unaanza kutaka kumkontrol, unawaza “Kama nisipomlinda huyu mwanaume basi nitampoteza:” Kwa maana hiyo unaanza kufuatilia simu zake. Kila dakika kumpigia simu kumuuliza kuwa yuko wapi? Hutaki awe na marafiki, kuna mdada ana mazoea naye unaanza kumchukia, kumuona kama adui anakunyang’anya bwana! Hutaki afanye baadhi ya vitu, labda kwenda Gym kwakua kuna wadada wazuri, unaanza kumkataza na kumpangia maisha. (3) Anachoka kuwa karibu na wewe, kwanza kwakua mwanaume hapendi kupangiwa maisha na kuendeshwa, Anaona kama unamchukulia kama mtoto na unataka kumkalia kichwani. Hapa moja kwa moja atafanya kila kitu ambacho unamkataza ili kuonyesha uanaume wake. Pili kwakua hatakusikkiliza utakua mtu wa hasira, kununa, kila akiwa na wewe hatafurahi tena kama mwanzo. Wewe unamlalamikia kabadilika na yeye anakulalamikia umebadilika, mwisho anaishia kukuacha kwakua hafurahii tena kuwa na wewe. Basi fahamu Kuwa, Chanzo cha migogoro ndani ya ndoa nyingi ni HISIA (DHANA) mbaya, Na hii inatokana pindi mmoja WA wanandoa anapomtilia shaka mwenza wake ktika jambo flani kisha akaifanya dhana hiyo Kuwa dira yake basi hapo iblis hakuachi salama lazima aichokonoe ndoa yako, Mume akichelewa kurudi kazini mke huanza kumfikiria vibaya mumewe "Kwa nin achelewe ilhali si kawaida yake?" basi hapo mke ataanza doria kama sungusungu ili kumchunguza mumewe Kumbuka mume hachungwi kama mbuzi Bali ni kumuomba mwenyezi MUNGU amlinde mwenza wako kwa kila Hali na wewe mwenyewe ukidumu katika kufanya ibada, Mungu hawezi kukupa mazuri tu wewe kila siku ilihali wewe unamchukiza, Mke usione kutumikia mumeo ni utumwa na kila kitu asaidiwe na msaidizi wa ndani, jitume Dada, Mume wako ndio Hatma yako, lazima umuhangaikie kwa jasho lako, Na udumu katika mambo haya, 1---Dumu Kuwa na haya kwa mumeo "Mwanaume hazoeleki." 2---Inamisha macho yako chini unapokuwa mbele ya mumeo, Mtazame kwa macho ya wizi aibu 3- Tii amri zake na unyamaze pindi anapozungumza mumeo, 4- Simama /msindikize mumeo pindi anapotoka nyumbani, japo uishie mlangoni tu, (sio mpaka mumeo anataka kwenda kazini wewe bado umejifunika shuka tu kitandani) 5- Mumeo anaporudi Simama mpokee, Na sio uwaachie watoto wako ndo wampokee au msichana WA kazi, ilhali wewe upo unaangalia tamthilia tu sebuleni, 6- Na ujiweke tayari kwa ajili ya mumeo pindi atakapokuhitaji, 7- Jipambe kana kwamba ndo unaolewa leo kwa kila aina ya manukato, Na uendelee kufanya Hivyo anapokuwepo mumeo na usiyafanye haya mume anapokuwa hayupo, (kasafiri) 8- Acha kufanya jeuri kwa mumeo (Kujifanya mgonjwa ili usimpe haki yake mumeo hata kama mlikwaruzana Muda mfupi uliopita,) 9- Jilinde mumeo anapokuwa mbali na wewe (kutokuzini) 10- Linda mali za mumeo wala usifanye matumizi mabay, Na uwakirimu ndugu wa mumeo, 11- Ukione kile kidogo anacholeta mumeo Kuwa ni kingi, Na utosheke na kile akupacho mumeo, 12- Usitoe Siri na mipango yenu ya maendele nje ya nyumba yenu 13- wala usitoke nyumbani ila kwa ruhsa ya mumeo,, (mwanamke asiyejitambua humdharau mumewe na hutoka Bila ruhsa ya mumewe,)
👍 ❤️ 🙏 4

Comments