Idara ya Habari - MAELEZO na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali
Idara ya Habari - MAELEZO na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali
May 21, 2025 at 11:56 AM
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa ametolea ufafanuzi juu ya uwepo wa taarifa za upotoshaji ulipjitokeza tarehe 20, Mei 2025 kupitia baadhi ya Akauti za mitandao ya kijamii kwa kuchapisha maudhui yenye lengo la kuzua taharuki na kuwajaza hofu wananchi. Msigwa ametoa ufafanuzi huo leo wakati akifungua mafunzo ya usalama mtandao (Cyber Security Awareness) kwa Wajumbe wa Kamati ya TEHAMA, Maafisa TEHAMA na Wawakilishi wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo yaliyofanyoka leo tarehe 21 Mei 2025 katika Ukumbi wa Jiji Dodoma
👍 ❤️ 🙏 8

Comments