
OFISI YA WAZIRI MKUU SERA BUNGE NA URATIBU
June 3, 2025 at 10:44 AM
“USHIRIKI WA TANZANIA JUKWAA LA DUNIA WAONGEZA FURSA ZA KIMATAIFA KUKABILIANA NA MAAFA” DK. YONAZI
TANZANIA imeshiriki Jukwaa la Nane la Dunia la Kupunguza Madhara ya Maafa lenye jukumu muhimu katika kuhamasisha na kukuza ushirikiano kati ya Serikali, Wadau na Mfumo wa Umoja wa Mataifa ili kuharakisha utekelezaji wa hatua za kupunguza madhara ya maafa.
Akizungumza wakati wa Mkutano huyo unaoendelea Mjini Geneva Uswisi kuanzia tarehe 02 hadi 6 Juni 2025, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri, Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Dkt.Jim Yonazi alisema jukwaa hilo ni chombo cha kutathmini, kujadili maendeleo ya utekelezaji na kuimarisha masuala ya usimamizi wa maafa kimataifa kupitia makubaliano ya hiyari ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa ambayo yameridhiwa na Makubaliano ya hiyari ya kimataifa yanayotekelezwa kwa sasa ni Mkakati wa Sendai wa Kupunguza Madhara ya Maafa 2015 – 2030
