
Samawati Safari
June 22, 2025 at 11:29 AM
Allen kila siku alikuwa akishuhudia pesa nyingi zikipita mbele ya macho yake ila ni pesa za watu na kuishia tu kuzitazama kwa macho
Hapa sasa ndipo likazaliwa wazo la kwanini asipige tukio akachukua kibunda na kutokomea pasipojulikana
Hili wazo aliishi nalo kwa mda mrefu sana.
Ila mpaka kufika mwaka 1996 hapo shetani aliweza kumvaa vyema na kuanza kulifanyia kazi wazo lake
Na katika kupanga mipango yake ni jambo moja tu ndo lilikuwa likimuumiza kichwa
Ni atawezaje kuvuka ulinzi mkali uliokuwa kwenye benk hiyo
Mwamba akaumiza sana kichwa bila ya majibu
