Find WhatsApp Channels

Discover the best WhatsApp channels for news, entertainment, education and more. Our powerful search helps you find exactly what you're looking for.

Channels & Posts for #assalaamair

Posts

Aviation Tanzania on Instagram: "As Salaam Air yaongeza ndege ya nne aina ya Embraer 120. Shirika la ndege la @assalaamairtz , lenye makao makuu visiwani Zanzibar, hivi karibuni limepokea ndege nyingine aina Embraer 120 yenye namba ya usajili 5H-LUF. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye mtandao wa Plane Spotter, ndege hiyo yenye iliwasili kwa mara ya kwanza katika Kisiwa cha Pemba juni 4 2025, ikitokea Zanzibar (ZNZ) na kutua salama katika Uwanja wa Ndege wa Pemba (PMA) majira ya saa 11:38 jioni Safari iliyochukua dakika 22 pekee. As Salaam ilianzishwa rasmi mwaka 2011 likifanya safari za Arusha-Zanzibar, Dar es Salaam-Pemba, Dar es Salaam-Zanzibar, Pemba-Dar es Salaam,Pemba-Zanzibar, Zanzibar-Arusha na Zanzibar-Pemba. Kwa sasa kampuni hiyo ina jumla ya ndege nne aina ya Embraer 120, kila moja ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 30. . #airline #assalaamair #fleetexpansion #newaircraft #assalaamair #embraer120 #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzania✈"

https://www.instagram.com/reel/DKrjPckNXRJ/?igsh=MWU4M2x4Nm0zMTNqcg== *As Salaam Air yaongeza ndege...

Aviation Tanzania on Instagram: "Assalaam Air Kushiriki Katika Maonyesho ya Kimataifa ya ITB 2025 nchini Ujerumani. Shirika la ndege nchini Tanzania la @assalaamairtz linatarajia kushiriki katika maonyesho ya kimataifa ya ITB Berlin kwa mwaka 2025. Ushiriki huu unatarajiwa kukuza mtandao wa shirika hilo na kuonyesha huduma maalumu za safari za ndani ya Tanzania pamoja na maeneo bora ya utalii nchini. Maonyesho hayo yatakayofanyika kuanzia Machi 4 hadi 6, 2025 katika mji wa Berlin nchini Ujerumani yatatoa fursa kwa shirika hilo kuungana na wateja wapya na kushiriki maarifa ya tasnia ya usafiri wa anga. Maonyesho ya ITB Berlin ni hafla kubwa zaidi ya biashara katika sekta ya usafiri, ambayo hufanyika kila mwaka, huzileta pamoja kampuni mbalimbali za usafiri, ikitoa fursa ya kipekee ya kujifunza kuhusu mwenendo wa hivi karibuni katika tasnia ya usafiri, kuimarisha uhusiano na mashirika ya kibiashara, na kuwasilisha huduma na bidhaa mpya za mashirika hayo. . #aviation #aviationlovers #avgeek #aircraft #newaircraft #assalaamair #embraer190 #aakia #tcaa #tanzaniaairportsauthority #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzania✈"

https://www.instagram.com/p/DGh3wSCtmya/?igsh=cHY0YXZwZ2psNGk1 *Assalaam Air Kushiriki Katika Maony...