RFI Kiswahili
                                
                                    
                                        
                                    
                                
                            
                            
                    
                                
                                
                                February 12, 2025 at 06:29 AM
                               
                            
                        
                            Waziri Mkuu wa Israel🇮🇱 Benjamin Netanyahu ameonya kuwa nchi yake itasitisha mkataba wa usitishwaji wa vita na kundi la Hamas, iwapo mateka wote wanaoendelea kushikiliwa hawatoachiliwa huru kufikia siku ya Jumamosi.
Kauli hii ya kiongozi huyo wa Israeli, inakuja baada ya rais wa Marekani🇺🇸 Donald Trump kuanza kutoa onyo hilo wiki hii.
Netanyahu amewaagiza wanajeshi wa Israeli kujiandaa kuendelea na vita kwenye ukanda wa Gaza.
Kundi la Hamas limetangaza kuwa limeahirisha zoezi la kuwaachia mateka kwa madai kuwa Israeli imekiuka masharti ya mkataba huo.
                        
                    
                    
                    
                    
                    
                                    
                                        
                                            👍
                                        
                                    
                                        
                                            ❤️
                                        
                                    
                                        
                                            😂
                                        
                                    
                                    
                                        5