
RFI Kiswahili
214.2K subscribers
Verified ChannelAbout RFI Kiswahili
Karibu katika chaneli ya Radio France International, idhaa ya Kiswahili. Fuatilia habari zetu kutoka Kila pembe ya Dunia.
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

Mamia ya raia wa jamii ya Ogale na Bille nchini Nigeria, wamewasilisha kesi mahakamani dhidi ya kampuni ya Shell wanayoituhumu kwa uchafuzi wa mazingira kupitia kuvuja kwa mabomba ya mafuta katika eneo la Niger delta,wakisema hilo limeathiri mfumo wao wa maisha . Kesi hiyo imewasilishwa katika mahakama ya London.


Magari ya Shirika la Msalaba Mwekundu yamefika katika eneo la pili huko Gaza, Nuseirat, katika Ukanda wa Gaza wa Kati, kwa ajili ya kukabidhiwa kwa wafungwa wa pii wa leo. Wafungwa wanne wa Kiyahudi kutoka Israeli wanaotarajiwa kuachiliwa na Hamas ni Hisham al-Sayed, ambaye alitekwa mwaka 2015 baada ya kuvuka mpaka kuingia Gaza peke yake, Omer Shem Tov, mwenye umri wa miaka 22, Eliya Cohen, mwenye umri wa miaka 27, na Omer Wenkert, mwenye umri wa miaka 23, ambao walitekwa kutoka kwenye tamasha la muziki la Nova tarehe 7 Oktoba 2023.


Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio na Rais wa Kenya William Ruto wamehimiza kusitishwa kwa mapigano mara moja mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wakati wa mazungumzo ya simu, Wizara ya Mambo ya Nje ilisema. Viongozi hao wawili walisisitiza dhamira yao ya kusukuma suluhu la kidiplomasia kwa mgogoro huo.


https://www.facebook.com/share/v/1EgM5gK2Xn/?mibextid=wwXIfr

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na Waziri Mkuu wa Uingereza Sir Keir Starmer hawajafanya lolote kumaliza vita nchini Ukraine, kabla ya ziara yao katika Ikulu ya White House wiki ijayo.


Uchunguzi kufuatia moto mkubwa ulioshuhudiwa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) nchini Kenya unaendelea. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Kenya (KAA), moto huo ulitokea kwenye eneo la nyasi linalozunguka uwanja huo. KAA imeeleza kuwa moto huo haukuathiri miundombinu muhimu wala shughuli za kawaida za uwanja wa ndege, na ratiba za ndege zinaendelea kama kawaida. Hii si mara ya kwanza kwa JKIA kukumbwa na tukio la moto. Mnamo Agosti 7, 2013, moto mkubwa ulizuka katika uwanja huo, na kusababisha kusitishwa kwa shughuli zote kwa muda.


Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov, ataitembelea Tehran hivi karibuni ili kukutana na mwenzake wa Iran kujadili mabadiliko na maendeleo ya kikanda na kimataifa. Imesema wizara ya Mambo ya Nje ya Iran.


https://www.youtube.com/live/jPRELzgqwy8?si=PP0bimL8jVY9fd93