
Swahili Times
February 12, 2025 at 03:18 PM
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime Rorya limesema limeanza uchunguzi wa kuwabaini watu watano wasiojulikana ambao wanatuhumiwa kuwakamata watu watatu wakazi wa Kijiji cha Itiryo Wilaya ya Kipolisi Nyamwaga.
Watu waliokamatwa na watu hao wanatambuliwa kama Muriba Muhere (41), Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi kata ya Itiryo, Lucas Chacha maarufu kama Kamanda (71) pamoja na Mwita Gesabo (45) wote wakazi wa Kijiji cha Itiryo.
Zaidi tembelea swahilitimes.co.tz
😂
👍
😮
❤️
😢
🙏
16