
Swahili Times
780.0K subscribers
Verified ChannelAbout Swahili Times
Habari | Elimu | Burudani | [email protected] | Maoni ya wasomaji si maoni ya Swahili Times | Simu/WhatsApp/Telegram: +255 743 778 779 | swahilitimes.co.tz
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

Mwigizaji wa Marekani, Tyler Perry ameshitakiwa na mwigizaji Derek Dixon kwa madai ya unyanyasaji wa kijinsia kazini, ambapo amedai fidia ya Dola milioni 260 [TZS bilioni 674.25]. Dixon anadai mara kadhaa Perry alifanya jaribio la kumbaka, na alipotaka kufichua matukio hayo, Perry alimpa ahadi ya kuendelea kumpa nafasi kwenye kipindi cha televisheni.


"Niongee na wazazi wenzangu, serikali tunatumia fedha nyingi kujenga shule za Msingi, Sekondari, za Ufundi na sasa tumeanza kuleta matawi ya vyuo vikuu katika mikoa mbalimbali, tafadhali wapeni vijana fursa ya kutumia fursa hizi za elimu ili wajijenge kwa maisha yao ya baadaye. " - Rais Samia Suluhu akiweka Jiwe la Msingi Shule ya Sekondari ya Amali Itilima


Viwango vya kubadilisha fedha za kigeni Juni 18, 2025.


Rais Samia Suluhu Hassan leo Juni 18, 2025 ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Amali ya Mwamapalala, iliyoko Wilaya ya Itilima, mkoani Simiyu. Rais Samia ameweka jiwe hilo la msingi kwa niaba ya shule zote 103 za Sekondari za Amali zinazojengwa nchi nzima.


"Tunamshukuru Mungu ametupa utajiri mkubwa wa vijana ndani ya Tanzania. Vijana hawa tusipowajengea uwezo, tusipowapa ujuzi uwezo wa serikali kuajiri wote haupo, ndiomaana tumeamua tuwape ujuzi, wawe mafundi waweze kujiajiri na kuajiriwa na sekta binafsi." - Rais Samia Suluhu akiweka Jiwe la Msingi Shule ya Sekondari ya Amali Itilima
