
JamiiForums
February 13, 2025 at 04:00 PM
Akizungumza katika mjadala wa "Kuelekea Uchaguzi, Tunatofautishaje Zawadi na Rushwa?" Wakili kutoka LHRC, William Maduhu, amesema suala la kutoa zawadi wakati wa Uchaguzi ni suala mtambuka, Miaka ya nyuma ilikuwa desturi kwa Mgombea yeyote kutoa zawadi kwa Wapigakura au Wananchi
Ameongeza “Mwaka 2005, LHRC ilitoa changamoto kuhusu suala hilo Kisheria Mahakamani, ndipo Mahakama Kuu ikaeleza kuwa kutoa takrima ni sehemu ya kushawishi Wapigakura. Baada ya hapo yakafuata mabadiliko ya Sheria yaliyoondoa vitu vinavyoweza kuchangia ushawishi kwa Wananchi wakati wa Uchaguzi”
Wakili Maduhu amesema pamoja na uwepo wa Sheria kadhaa kupinga viashiria vya Rushwa Nchini lakini matukio ya Wagombea au watia nia kuendelea kutoa zawadi kwa Wapigakura bado yapo
😂
🙏
2