JamiiForums WhatsApp Channel

JamiiForums

716.2K subscribers

Verified Channel

About JamiiForums

Karibu katika Chaneli yetu rasmi ndani ya WhatsApp. Pata taarifa za uhakika, kwa wakati | Tanzania

Similar Channels

Swipe to see more

Posts

JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 9:26:04 AM

DODOMA: Mdau wa JamiiForums.com anaeleza kuwa Daraja lililopo Kata ya Mkonze, Mtaa wa Muungano linalounganisha Mtaa wa Muungano na Goba limeharibika na halijafanyiwa maboresho kwa muda mrefu Anadai vyombo vyote vya usafiri na wanaotembea kwa miguu wanalazimika kupita pembeni kwa kuwa eneo la katikati halipitiki Anaongeza kuwa ikinyesha mvua ukiwa upande mmoja kati ya maeneo hayo lazima usubiri mpaka maji yapungue ndio uvuke, anatoa wito kuwa Daraja liboreshwe kwa kuwa hali ilivyo ni mateso kwa wapitaji wa hapo Soma https://jamii.app/DarajaLaMuunganoGoba

🙏 ❤️ 👍 4
Video
JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 8:44:08 AM

DAR: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mifumo ya Hali ya Hewa haioneshi uwepo wa mvua hivi karibuni hapa nchini badala yake kutakuwa na ukavu na ubaridi ambapo Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari za kujilinda na baridi Meneja wa Utabiri wa TMA, Dkt. Mafuru Kantamla amesema mvua zilizonyesha hivi karibuni Ukanda wa Pwani zimetokana na ongezeko la Joto katika Bahari ya Hindi hususan katika Mwambao wa Pwani lakini hazitakuwa na mwendelezo kwa kuwa joto la Bahari limeanza kupungua kwa kasi Soma https://jamii.app/HaliYaHewaJuni Video Credits: Torch Media

👍 😂 ❤️ 😢 🙏 🫡 16
Video
JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 12:10:53 PM

SONGWE: Mdau anadai changamoto ya foleni ya magari ya mizigo mpaka wa Tanzania na Zambia upande wa Tunduma ni kero kubwa, inakwamisha Uchumi wa Watu wengi na kuwafaidisha wachache Anadai kuna Kiongozi wa Usalama hapo anamiliki eneo la kuegesha (parking) anatoza Sh 10,000 kwa siku badala ya Tsh. 5,000 inayotozwa kwingine na kwamba Mwanausalama huyo anatoa kipaumbele kwa Wateja wake kuvusha magari huku wengine wakibaki kucheleweshewa mchakato Pia, Mdau anadai hali ya Watumishi kukosa uadilifu inachangia foleni kwa kuwa michakato inafanyika kwa kasi ndogo kwa baadhi ya Maafisa kujali maslahi binafsi Ikumbukwe, Aprili 2025, Mkuu wa Mkoa, Daniel Chongolo aliunda Kamati Maalumu kuchunguza msongamano huo ambapo baadhi ya Wadau walimwambia inatengenezwa na Watu wachache kwa sababu wanazozijua wao Soma https://jamii.app/TundumaFoleniJuni Video Credits: CHAWAMATA TV

👍 😂 😮 😢 ❤️ 16
Video
JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 10:37:26 AM

KENYA: Maafisa Polisi wamemkamata Askari anayefahamika James Mukhwana kwa kuhusika na mauaji ya cha mwalimu na mwanablogu, Albert Omondi Ojwang' aliyefariki akiwa kizuizini baada ya kushikiliwa kwa kuchapisha taarifa za uongo Kwa mujibu wa ripoti ya Polisi imesema kuwa Askari James wa Kituo cha Polisi cha Kati Nairobi alikamatwa Juni 12, 2025 na kuwekwa rumande katika Kituo cha Polisi cha Capitol Hill na anatarajiwa kushtakiwa kwa kosa la mauaji ya Ojwang' Ikumbukwe Albert Ojwang' (Mwanaharakati na Mwanamtandao) alifariki Dunia Juni 8, 2025, Siku moja baada ya kukamatwa Nyumbani kwake Kakot, Homa Bay, akiwa chini ya uchunguzi kuhusu chapisho alilodaiwa kumdhalilisha Naibu Mkuu wa Polisi kwenye Mtandao wa Kijamii wa X Soma https://jamii.app/AskariJamesKifoOjwang

Post image
👍 😂 ✌️ ❤️ 😢 😮 🙏 14
Image
JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 6:29:21 AM

DIPLOMASIA: Israel imefanya mashambulizi Nchini Iran katika Mji wa Tehran ikiwa ni sehemu ya Oparesheni kwa kile ambacho Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amesema walilenga kudhoofisha Miundombinu ya Nyuklia ya Iran na Viwanda vya Makombora ya masafa marefu Pamoja na hivyo, Israel imetangaza hali ya hatari, ikisema inatarajia mashambulizi ya kulipiza kisasi kutoka kwa Iran, wakati ambapo Iran imesema mashambulizi hayo yameathiri Makazi ya raia na kuua Watu kadhaa wakiwemo Watoto Wakati huohuo, Rais wa Marekani, Donald Trump amekiambia Kituo cha Fox News kuwa alikuwa na taarifa kuhusu mashambulizi hayo kabla lakini Nchi yake haikuhusika kwa namna yoyote Soma https://jamii.app/IsraelAgainstIran

👍 😡 😂 😅 😢 😮 🖕 😳 16
Video
JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 11:23:35 AM

DAR: Klabu ya Simba imesema Serikali imeruhusu watumie Uwanja wa Mkapa kufanya mazoezi Juni 14, 2025 ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Yanga unaoratajiwa kuchezwa Juni 15, 2025 Barua hiyo imeeleza kuwa uwanja upo tayari kwa mchezo na wameruhusiwa kwa mujibu wa Kanuni kwa kuwa Simba itakuwa ugenini katika mchezo huo ambao Yanga imekuwa ikisisitiza haitaingiza timu uwanjani Barua imeandikwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Boniface Tamba kwenda kwa Simba na nakala kwa Afisa Mtendaji wa Bodi ya Ligi Kuu Soma https://jamii.app/SimbaMazoezi

Post image
😂 🙏 ❤️ 👍 🔥 🖕 😏 😮 🦁 33
Image
JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 1:11:39 PM
Post image
😂 😢 2
Image
JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 1:11:32 PM
Post image
😂 4
Image
JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 7:19:39 AM

UTEUZI: Rais Samia amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani, George Mcheche Masaju kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, akichukua nafasi ya Prof. Ibrahim Hamis Juma ambaye amestaafu Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Moses Kusiluka, imeeleza uapisho wa Jaji Mkuu utafanyika Juni 15, 2025 Ikulu, Chamwino - Dodoma, Saa 4.00 Asubuhi Soma https://jamii.app/UteuziGeorgeMcheche

Post image
😂 🙏 ❤️ 👍 😢 🌳 🎉 👏 🤨 29
Image
JamiiForums
JamiiForums
6/13/2025, 4:50:30 AM

Kukosea siyo tu jambo la kawaida, bali pia ni muhimu sana kwa ukuaji na kujifunza. Tunajifunza kutokana na makosa yetu, tunaboresha ujuzi wetu na tunakuwa watu wenye Hekima zaidi. Makosa yanatuonesha pale tulipofanya vibaya na kutupa fursa ya kurekebisha na kusonga mbele.

Post image
👍 ❤️ 🙏 🤝 👊 👏 📌 😮 52
Image
Link copied to clipboard!