
JamiiForums
February 13, 2025 at 05:01 PM
Akizungumza katika mjadala wa "Kuelekea Uchaguzi, Tunatofautishaje Zawadi na Rushwa?", Mwenyekiti wa Bodi (JUKATA), Dkt. Ananilea Nkya, amesema “Suala la Rushwa kabla ya Mwaka 2005, Rushwa ilikuwa inafanyika waziwazi kwa kutumia jina la Takrima ikiwa ni kama Zawadi ya waziwazi. Baadaye Sheria ikasema hiyo siyo Zawadi bali ni Rushwa, lakini mtazamo wangu ni kuwa Rushwa imeongezeka kuliko ilivyokuwa awali ”
Ameongeza kuwa “Watu wengi wanailaumu TAKUKURU, Mimi nasema tusiwalaumu wao kwa kuwa zamani Rushwa ilitolewa waziwazi kwa jina la Takrima tofauti na sasa ambapo inafanyika kwa usiri mkubwa”
Amesema zamani Rushwa ilikuwa inaweza kutolewa kwa njia ya Chakula, Nguo au kitu kingine chochote cha kuwahadaa Wananchi lakini sasa hivi Rushwa inatolewa kwa ukubwa zaidi na kwa kificho kiasi kwamba TAKUKURU ni ngumu kuweza kumkamata Mtu sababu mambo mengi yanafanyika gizani
😂
2