
JamiiForums
February 13, 2025 at 05:06 PM
Mwenyekiti wa Bodi (JUKATA), Dkt. Ananilea Nkya, amesema Chanzo cha Rushwa katika Uchaguzi ni kutokana na kukosekana kwa Mifumo sahihi ndani ya Chama ya kupatikana kwa Viongozi
Ameongeza “Ili Mtu apate Uongozi ni lazima awe na uwezo wa kuwahonga au kuwapa Rushwa Wajumbe, hiyo inamaanisha yeyote ambaye hana uwezo wa kuwapa Rushwa Wajumbe anakuwa hana nafasi”
Amesema Rushwa haiwezi kuondoka au kupungua kama Mifumo ya kupata Viongozi ndani ya Vyama haitakuwa na mabadiliko, tutakuwa tunaenda mbele na kurudi nyuma na pengine hali kuwa mbaya zaidi
❤️
🙏
👍
6