JamiiForums
                                
                                    
                                        
                                    
                                
                            
                            
                    
                                
                                
                                February 13, 2025 at 05:26 PM
                               
                            
                        
                            Wakili William Maduhu (LHRC) amesema “Kuna wakati Viongozi wanatumia Madaraka yao kutoa ahadi na kutoa vitisho kwa Wananchi kuwa hawatakiwi kuwachagua wapinzani wakati wa Uchaguzi lakini huwezi kuwasikia TAKUKURU wakiingilia kati hapo”
Amesisitiza kwa kutolea mfano Wabunge wa sasa waliopo Madarakani wanaenda kwenye Majimbo kutoa vitu mbalimbali ikiwemo Pikipiki, Baiskeli n.k. lakini watia nia wengine wakienda kufanya hivyo TAKUKURU wanawakamata
Ameongeza kuwa “Inavyofanyika ni kuwa Mbunge ambaye ana nia ya kugombea tena akifanya hivyo ni sawa lakini yule mwenye nia ya kugombea yeye akifanya hivyo anaambiwa anatoa Rushwa
                        
                    
                    
                    
                    
                    
                                    
                                        
                                            ❤️
                                        
                                    
                                        
                                            😂
                                        
                                    
                                        
                                            😢
                                        
                                    
                                    
                                        5