
JamiiForums
February 13, 2025 at 05:36 PM
Mwanasiasa (ACT Wazalendo), Zitto Kabwe amesema “Wakati wa Kura za maoni za CCM huwa ni kawaida kuwasikia sana TAKUKURU lakini baada ya hapo huwezi kuwasikia tena”
Ameongeza kwa kusema “TAKUKURU ni kama wanakuwa na jukumu la kudhibiti Rushwa ndani ya CCM lakini huwaoni wakati wa Uchaguzi Mkuu, hata unapotoa taarifa kwa Mamlaka nyingine za Usalama, inachukuliwa kawaida kwa maana hakuna anayechukua hatua”
Amesema kuwa kwa sasa sio mjadala tena kuwa kuna Rushwa au hakuna wakati wa Uchaguzi, inajulikana kinachoendelea
👍
❤️
🙏
8