
TheChanzo
February 3, 2025 at 09:44 AM
*Ifike Wakati Maofisa Habari wa Klabu Waache Kupumbaza Mashabiki wa Soka*
*Na Angetile Osiah*
Kuna aina ya uvivu imeingia kwenye vyumba vya habari, hasa katika madawati ya michezo ambako hivi sasa wale watu rasmi, kama viongozi, makocha na wachezaji si muhimu katika utoaji habari, bali watu wanaoweza kuchekesha, au kusema magumu ambayo mtu anayewajibika katika taasisi hawezi kusema.
Mtu ambaye anasema anamuweka rehani mke wake iwapo timu fulani itashinda, si mtu anayewajibika kwa taasisi, jamii, na hasa familia yake.
Mtu anayesema timu yake ilipiga pasi milioni 90, hawezi kuwa anawajibika kwa taasisi yake, au chombo kingine chochote, kwa kuwa anazungumzia kitu ambacho hakiwezi kutokea kwenye mchezo wa mpira wa miguu.
Soma https://thechanzo.com/2025/02/03/ifike-wakati-maofisa-habari-wa-klabu-waache-kupumbaza-mashabiki-wa-soka/
👍
😂
🙏
3