
JamiiForums
February 27, 2025 at 05:49 PM
Akichangia mjadala Francis Nyonzo (Mdau) amesema kuwa inatakiwa watu wafundishe kuwa na msimamo wa kusimamia kile wanachokiamini, hilo linatakiwa kwenda pamoja na Utawala wa Sheria
Ameongeza kwa kusema Uchawa ni kusifia tu hata kama jambo sio la kusifia, mfano tabia ya Watoto kuwa na utii bila kutoa hoja imekuwa ikitengenezwa na Wazazi na Walezi, kadiri inavyokuwa inamtengeneza Mtoto ambaye hawezi kubishana kwa hoja

👍
❤️
😮
🙏
6