Ashraf JK 💚💙
Ashraf JK 💚💙
February 25, 2025 at 07:39 AM
Baraza Kuu la Famasi la Uingereza (GPhC) limeweka masharti mapya magumu kwa maduka ya dawa ya mtandaoni yanayouza sindano za kupunguza uzito kama Wegovy na Mounjaro. Hatua hii inalenga kuzuia watu wenye uzito wa kawaida au wenye historia ya matatizo ya kula kupata dawa hizi kwa urahisi. Sasa, wagonjwa watahitaji kufanyiwa mashauriano ya ana kwa ana au kwa video, badala ya kujaza dodoso mtandaoni au kutuma picha. Aidha, taarifa zao za afya zitapaswa kuthibitishwa kutoka kwa daktari wao wa familia. Maduka ya dawa yanayokiuka masharti haya yanaweza kuchukuliwa hatua za kinidhamu, ikiwa ni pamoja na uchunguzi wa kitaaluma au mipango ya maboresho. GPhC imeeleza wasiwasi wake kuhusu utoaji holela wa dawa hizi na shinikizo kwa wafamasia kufanikisha maagizo mengi kwa muda mfupi. Dawa hizi, awali zikitumika kwa wagonjwa wa kisukari cha Aina ya 2, sasa zinachukuliwa kuwa "hatari kubwa" kutokana na upatikanaji wake mdogo na ongezeko la bidhaa bandia. Tafiti zinaonyesha kuwa, mbali na kupunguza uzito, dawa hizi pia zinaweza kuboresha afya ya moyo kwa kupunguza hatari ya shinikizo la damu, mshtuko wa moyo, na kiharusi. #kmt #ashrafjk #afyatamu

Comments