NURU YA UPENDO
NURU YA UPENDO
February 13, 2025 at 02:11 PM
https://wingulamashahidi.org/2022/09/21/kanuni-rahisi-ya-kupokea-baraka-mara-dufu/ *KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.* Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, Mkuu wa mbingu na nchi libarikiwe. Kitabu pekee chenye mwongozo kamili wa maisha ni biblia takatifu, Mtu mmoja wa Mungu aliwahi kusema “endapo nikifungiwa katika chumba chenye giza, nikapewa mshumaa na biblia, basi ninaweza kueleza yote yanayoendelea nje katika ulimwengu”. Hakika hiyo ni kweli kabisa..kwasababu biblia ndio kitabu pekee kinachoelezea uhalisia wa nyakati na majira tunayoishi, na mambo yajayo.. Leo napenda tujifunze kanuni moja rahisi ya kupokea baraka..Wengi wetu, tunategemea maombi tu, tunakuwa tunatumia nguvu nyingi katika kuomba ili kusudui tupokee baraka katika mwili, lakini ipo kanuni moja rahisi ya kupokea baraka.. Na kanuni hiyo Bwana Yesu aliisema katika Marko 4:24.. Marko 4:24 “Akawaambia, Angalieni msikialo; kipimo kile mpimacho NDICHO MTAKACHOPIMIWA, na TENA MTAZIDISHIWA”. Hapo nataka tuyatazame hayo maneno miwili. 1)Kipimo mpimacho ndicho mtakachopimiwa. na 2) tena mtazidishiwa Maana yake ni kwamba Kama utampimia mwingine kwa kumpa “sh.elfu moja”..basi Bwana atahakikisha anakurudishia kwa njia nyingine hiyo “elfu moja” uliyoitoa. (Huenda ikawa siku hiyo hiyo, au wakati mwingine ambao haupo mbali sana). Lakini haiishii hapo tu kukurudishia hiyo elfu moja..bali anaendelea kwa kusema “na tena mtazidishiwa”. Ikiwa na maana kuwa Bwana akishakurudishia kile ulichokitoa, sasa kinachofuata ni yeye kukulipa wema ulioufanya kwa “kwa kukuzidishia”. Maana yake atakupa na kingine kingi zaidi ya hiyo elfu moja uliyoitoa, Sasa ili tuelewe vizuri ni kiasi gani tutazidishiwa, hebu tuyatazame tena maneno ya Bwana Yesu katika Luka 6:38. Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”. Hapa nataka tuugawanye tena mstari huu katika sehemu mbili. 1) Wapeni watu vitu nanyi mtapewa na 2) Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa kifuani mwenu. Maana yake tunapowapa watu, kipimo fulani labda elfu moja na sisi Bwana ataturudishia hichohicho kipimo
🙏 1

Comments