
NURU YA UPENDO
21.1K subscribers
About NURU YA UPENDO
Karibu katika channel yetu, ya mafundisho ya Neno la Mungu ya Kila siku. Kwa msaada wa kiroho/ kuchangia kazi ya MUNGU, wasiliana nasi kwa namba hizi +255693036618/ +255789001312
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

*MAOMBI YA USIKU.* JUMATATU[09.06.2025] JINA LA BWANA WETU YESU KRISTO LIBARIKIWE SANA. KARIBU KATIKA MAOMBI YA USIKU VIPENGELE VITATUMWA KILA SIKU USIKU UNAOMBA WAKATI WA KULALA UKISHAMALIZA KULA CHAKULA CHAKO SIO MAOMBI YA MFUNGO . ● *MAOMBI YA LEO JUMATATU TUTAOMBA KUHUSIANA NA ULINZI WA KIROHO NA KIMWILI KATIKA MAISHA YETU* . *MShukuru Mungu kwa siku Ya Leo . zaburi 118:1 ,118:21. *Omba Toba na Rehema. Zab 51:1_4. *Omba Utakaso wa Nafsi ,Roho Na Mwili kwa Damu Ya Yesu.1 Wathesalonike 5:23 >Fungua wiki hii kwa Damu Ya Yesu Kuanzia Jumatatu Ya leo Mpaka jumapili Ya 15.06.2025 na Tamka milango Ya Baraka na Baraka zote za kiroho zifunguke kwa Jina la Yesu. >Funga roho za wachawi, mauti, magonjwa ,ajali, vifo vya ghafla, vizuizi vya maendeleo visipate nafasi kwa Jina la Yesu. 1.Omba wigo wa Bwana Uifunike familia Yako.OMBEA WENGINE HILO HITAJI. Ayubu 1:10. 2.omba Malaika Wa Bwana Watembee na Ndugu ,jamaa, Marafiki ,zako .OMBEA WENGINE HILO HITAJI. 2 Wafalme 6:17. 3.omba Ulinzi wa Kimungu katika Mazingira yote na mahali ulipo ukawepo masaa ishirini na nne[Mchana na Usiku].OMBEA WENGINE HILO HITAJI.zab 91:4_5. 4.Omba Mungu akuokoe dhidi Ya hila za Adui katika Maisha Yako .OMBEA WENGINE HILO HITAJI.Zab 91:3 5.Ombea Majaribu Mbalimbali Ya Adui Mfano Ya Ayubu Yasizuke kwenye Familia yako kama ajali, Majanga ,Vifo vya Ghaflan.kOMBEA WENGINE HILO HITAJI. Luka 22:40. ■VUNJA NA KUHARIBU ROHO ZA WACHAWI, MAGONJWA ,MAUTI, NGUVU ZA GIZA, LAANA ,MAAGANO KATIKA JINA LA YESU NA ACHILIA DAMU YESU KWA FAMILIA, KAZI ,KANISA ,TAIFA ,WATOTO , VIJANA ITUME DAMU YA YESU USIKU WA LEO. N.B. KUOMBA NI MUHIMU[MITHALI 16:1]. MUNGU AKUBARIKI.

*MAOMBI YA USIKU.* JUMANNE[10.06.2025]. JINA LA BWANA WETU YESU KRISTO LIBARIKIWE SANA. KARIBU KATIKA MAOMBI YA USIKU VIPENGELE VITATUMWA KILA SIKU USIKU UNAOMBA WAKATI WA KULALA UKISHAMALIZA KULA CHAKULA CHAKO SIO MAOMBI YA MFUNGO. *NENO KUU*: *KWA NEEMA TUNAOKOLEWA.* Marko 8:22-26 "Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, akamtemea mate ya macho, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu? -Akatazama juu, akasema, Naona watu kama miti, inakwenda.Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, naye akatazama sana; akawa mzima, akaona vyote waziwazi.Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie." .✓ *VIPENGELE VYA MAOMBI YA LEO JUMANNE.TUNAOMBA* *KWA AJILI YA NEEMA TELE.* ✓Mshukuru Mungu Kwa Ulinzi ,Uzima na Nguvu , Kwa Taifa,familia , Makanisa, viongozi,Huduma,BiasharaKadiri Roho Mtakatifu atakavyokuongoza *Zaburi 92:1-2.* ✓ Omba Toba Na Rehema juu ya Makanisa, Familia ,Watoto , Nchi,Watumishi , ZABURI 51:4 ✓Omba Utakaso Wa Nafsi, roho na Mwili . 1Wathesalonike 5:23. 1•Omba Bwana Akusaidie upate kibali machoni pake. omba neema iongezeke kwako, familia yako, katika huduma , biashara , kazi, elimu, nk. 2 Kor 12 : 9. Mwanzo 39 : 4..ombea na Wengine Kwa Hilo Hitaji. 2•. 1 Wakorintho 15 : 10. Niko hivi nilivyo kwa neema yako. Naomba kibali chako katika maisha yangu,. Naomba neema yako katika maisha yangu isiwe bure.ombea na Wengine . 3• Napokea kibali na milango itafunguka kuanzia sasa kwa Jina la Yesu .Dan 1 : 9. • Kibali cha Bwana kifungue milango Ya Kazi,Elimu ,Biashara, Uongozi , Utumishi , iliyokua imefungwa katika jina Yesu. • Kila mlima ulio simama mbele yangu na ung’oke kwa jina la Yesu. Zakaria 4: 6, Zaburi 84 : 11. •Bwana wewe ni jua langu na ngome yangu,kila jambo jema litaachiliwa kwangu mwaka huu katika jina la Yesu.OMBEA NA WENGINE KWA HILO HITAJI. 4• Kama kanisa tusaidie kutembea katika neema yako,tupe neema ya kuongezeka,kuinuliwa na kupanda juu katika jina la Yesu. Zaburi 75 : 6. Tamka Kanisa unaposalia, Na Usisahau na Kutaja Kanisa la Nuru Ya Upendo Neema Ya Mungu Ikawepo. 5•. Kwa neema yako dhambi haina nguvu juu yangu tena. Warumi 6 : 1-14. Warumi 7:1-23. Ombea na Wengine . *N.B* Vipengele vya Maombi Mungu Akipenda Tutaona Kesho. ✍🏽 *NA IKIWA UNAHITAJI LAKO LA KUSHIRIKISHANA, MAOMBEZI, KUOKOKA, UKIONA AMANI TUMA. *_[Wagalatia 6:2]_* *Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.* *_[Wakolosai 3:15 ]_* **Na amani ya Kristo iamue ndani yenu,ndiyo mliyo itiwa katika mwili mmoja* . 0793006146 . ✓Mungu akubariki.

https://wingulamashahidi.org/2023/04/06/ninyi-akina-baba-msiwachokoze-watoto-wenu/ *NINYI AKINA BABA MSIWACHOKOZE WATOTO WENU* Majukumu ya Mzazi ni kumlea mtoto katika njia inayompasa, kwasababu hekima ya Mungu inasema, hataiacha njia hiyo hata atakapokuwa mzee. Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee” Lakini pamoja na kumlea mtoto katika njia impasayo ya kiMungu, mzazi pia hapaswi kumchokoza mwanae sawasawa na maandiko yafuatayo… Waefeso 6:4 “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana”. Wakolosai 3:21 “Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa” Sasa utauliza nini maana ya kuchokoza? Kuchokoza kama ilivyotumika hapo, ni “kitendo cha kumfanya mtoto awake hasira, pasipo kuwa na sababu ya msingi” Na baadhi ya sababu hizo ambazo zinaweza kumfanya mtoto awake hasira, hata kufikia hatua ya kukata tamaa au kufanya dhambi kama za kutoa maneno mabaya mdomoni au moyoni..ni kama zifuatazo. 1.Ukali wa mzazi uliopitiliza. Mzazi anapokuwa mtu wa kufoka mara kwa mara, na kushutumu kwa ukali mambo yasiyo na mashiko ni rahisi kumfanya mtoto akate tamaa au awake hasira, na kitendo hicho kibiblia kinatafsirika kama “Mzazi kamchokoza mwanae”. 2. Kumwadhibu mtoto mara kwa mara bila kuwa na sababu ya msingi. Wapo wazazi ambao mtoto akifanya kosa dogo tu, tayari wamekamata kiboko na kutoa adhabu kali. Ni lazima mzazi apime kosa, kama linastahili adhabu au linastahili kuonya tu!.. Lakini sio kila kosa hukumu yake iwe viboko!. Hilo linaweza kumfanya mtoto achukizwe sana badala ya kujengeka, na kibiblia ikahesabika kama umemchokoza mwanao na si kumjenga. 3. Kumdhalilisha mtoto Wapo wazazi wasiowatia moyo watoto wao, badala yake wanawadhalilisha mbele ya watoto wenzao, au mbele ya jamii.. Jambo kama hili pia kibiblia linatafsirika kama mzazi kamchokoza mwanae. Tunapaswa siku zote kuwathaminisha watoto wetu mbele ya watoto wengine, vile vile kuwatia moyo katika mambo mazuri wanayoyafanya. Na wazazi wengi hawajui kama wanawachokoza watoto wao, na kuwaharibu utu wao wa ndani kwa ukali wao. Hivyo kama mzazi, zingatia mambo hayo (Usiwachokoze watoto wako) na Bwana atakubariki na vile vile kuwabariki watoto wako. Bwana akubariki. Tafadhali shea na wengine ujumbe huu; Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: *+255693036618 au +255789001312*


https://wingulamashahidi.org/2024/02/06/baraka-za-wazazi-kwa-watoto/ *BARAKA ZA WAZAZI KWA WATOTO.* Masomo maalumu kwa wazazi/walezi. Je unazijua kanuni za kuwabariki watoto wako?.. Wengi tunaijua kanuni moja tu ya kuwatamkia Baraka!..Hiyo ni sahihi kabisa na ipo kibiblia..(kwasababu maneno ya kinywa yana nguvu). Lakini ni vizuri kufahamu jambo moja, kama Maneno yako hayataambatana na matendo yako, uwezekano wa hayo uliyoyasema kutokea bado utakuwa ni mdogo sana. Kama unataka mtoto wako apate Baraka zote ulizozitamka juu yake, (na kwa njia ya maombi) ikiwemo Baraka katika kumjua Mungu, kuwa na afya na mafanikio, basi ongezea yafuatayo.. 1.MFUNDISHE SHERIA ZA MUNGU. Wafundishe watoto wako sheria za Mungu, huku wewe mwenyewe ukiwa kielelezo cha kuzifanya, ili wasione kama ni sheria tu za MUNGU bali hata zako wewe mzazi!.. Mtoto wako anapaswa azione sheria za Mungu kama ni za kwako wewe. Lakini asipoona wewe mwenyewe ukizifanya hata yeye hataweza kukusikiliza wala kuzitenda, hata kama kwa mdomo atakuitikia. Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako, 9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”. 2. USIMNYIME MAPIGO. Yapo makosa yanayoweza kurekebishwa kwa maneno peke yake na mtoto akajengeka na kubadilika, lakini yapo yanayohitaji kurekebishwa kwa maneno pamoja na kiboko, hususani yale ya kujirudia rudia tena ya makusudi. Biblia inasema ukimpiga hatakufa bali utakuwa umemwokoa roho yake na kuzimu.. (Hapo utakuwa umembariki pakubwa Zaidi ya kumtamkia tu baraka za maneno halafu hufanyi chochote). Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. 14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”. 3. MFUNDISHE KUSHIKA ELIMU Badala ya kumtakia tu Baraka kwa kinywa (au kumwombea tu katika chumba chako cha ndani), tenga muda wa kumfundisha Umuhimu wa Elimu (kwanza ya Mungu) na pili ya dunia… Hapo utakuwa umembariki kwa vitendo na si mdomo tu. Mithali 4:13 “Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako” 4. MFUNDISHE KUSHIKA SHERIA ZA NCHI na KUWAHESHIMU WENYE MAMLAKA (Wafalme). Badala ya kumtamkia tu mafanikio, na kumwombea.. tenga muda kumfundisha umuhimu wa kuwatii wenye mamlaka na kuzingatia sheria ya nchi, hiyo itakuwa Baraka kwake katika siku zijazo za maisha yake. Mithali 24:21 “Mwanangu, mche Bwana, NA MFALME; Wala usishirikiane na wenye kigeugeu; 5. MFUNDISHE KATIKA NJIA INAYOMPASA Ni njia gani inampasa katika umri wake na jinsia yake?.. Je! Katika umri wake huo anapaswa amiliki simu??..je katika umri wake anapaswa asemeshwe maneno hayo unayomsemesha?..je katika umri wake anapaswa atazame hayo anayoyatazama katika TV?.. je katika umri wake huo anapaswa awepo hapo alipo?..anapaswa afanye hicho anachokifanya?.Je! Kwa jinsia yake anapaswa kuvaa hayo mavazi unayomvika??.. Ni muhimu sana kujua mambo yampasayo mwanao/wanao kwa rika walilopo na jinsia zao… Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee” Ukiyafanya hayo na mengine kama hayo pamoja na MAOMBI umwombeayo kila siku, basi utakuwa umembariki mwanao/wanao kweli kweli. Bwana akubariki. Tafadhali shea na wengine ujumbe huu; Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
