NURU YA UPENDO
NURU YA UPENDO
February 19, 2025 at 04:13 PM
*MAOMBI YA USIKU* ( *JUMATANO 19.02.2025).* Shalom.Shalom. *NENO KUU* : *KUTAFUTA AMANI* : Waebrania 12:14. "Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;" ✓ Mshukuru Mungu Kwa Makanisa, Familia, Taifa ,Afya , Nguvu ya Maombi kila siku Usiku anazokupa kuomba . ✓Omba Toba na Rehema . ✓Omba Utakaso Wa Roho ,Nafsi na Mwili . *VIPENGELE VYA MAOMBI LEO JUMATANO* *KUHUSIANA NA KAZI ZINAZOTUINGIZIA KIPATO(Uchumi &Fedha ).👇👇* Muendelezo---. ■ *OMBA NGUVU YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO ILI IKUSAIDIE KUMPASUA SIMBA ALIYE UTISHO KWAKO* ( Yaani hali mbaya ya kiuchumi iliyo UTISHO kwako ) na ILIYOSHIKILIA ASALI YAKO. Kumbuka simba aliye uawa na Samsoni ndiye alikuwa amebeba ASALI. [ Asali =Uchumi, Fedha, Faida ] ●Roho ya Nguvu iliyomuijia Samsoni ndiyo iliyompa uwezo wa kumrarua simba na kula Asali akawapa na ndugu zake. ** *Omba ManenoHaya Kwa kumaanisha 👇* ✓Vunja kila roho iliyoshikilia Uchumi wako na biashara zako na Faida zako Kwa Jina la Yesu na Achilia Damu Ya Yesu . ■Navunja kila nguvu ya giza kwenye kazi zangu Kwa Jina la Yesu . ■Nakataa Kila roho ya Upofu kwenye kazi zangu Kwa Jina La Yesu ■Naipinga roho ya uvivu na ulegevu kwenye kazi zangu Kwa Jina La Yesu. ■Naharibu kila madhabahu ya Giza kazini kwangu Kwa Jina La Yesu . ■Roho ya Kupoteza naipinga kwa Jina la Yesu. ■Roho ya ugumu ninaiondoa kwa Jina la Yesu. ■Kila mawasiliano ya giza ofisi kwangu nayakata kwa Jina la Yesu. ■Natamka Neema na Baraka kazini kwangu Kwa Jina La Yesu . " Roho ya BWANA ikamjilia kwa nguvu, naye akampasua kana kwamba anampasua mwana-mbuzi, wala hakuwa na kitu cho chote mkononi mwake; lakini hakuwaambia baba yake na mama yake aliyoyafanya." Waamuzi 14 :6 ●Hiyo Roho ya Nguvu ndiyo ukupayo Utajiri na fedha. "Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo." KUM 8:18 **Omba ManenoHaya Kwa kumaanisha 👇* ✓Mwambie Mungu akupe Nguvu za kusonga Mbele. ●Bwana Yesu naomba nijaze nguvu ndani yangu ●Naomba nguvu Katika, roho ,Mwili nafsi yangu ●Naomba nguvu Katika fikira, na mawazo yangu ●Naomba Nguvu Katika Nafasi Yangu ●Naomba nguvu zako katikati ya maadui Zangu Isaya 62:7-8 ●Naomba nguvu za Roho Mtakatifu Kwenye maamuzi yangu na matumizi yangu ya fedha. ●Mungu naomba nguvu zako kwenye kazi zangu ●Mungu nivike nguvu kwenye mikono yangu ●Kazi yangu ikawe na kibali kikuuu ●Neema ya nguvu KATIKA mambo magumu ikae ndani yangu ●Naomba nguvu ya fedha na utajiri. ●Aminaaa ■ *MWAMBIE MUNGU MANENO YAKO YAPATE KIBALI MBELE ZAKE.* Maneno ya kinywa changu,Na mawazo ya moyo wangu,Yapate kibali mbele zako, Ee BWANA,Mwamba " Zaburi 19:14 Chochote ukichomueleza Mungu kwenye maombi haya na kikapate KIBALI mbele zake na Kukujibu. Amina. ■Mungu akubariki.
🙏 😂 4

Comments