
๐ข๐ง๐๐จ๐ ๐๐ก ๐๐๐๐ง
February 3, 2025 at 12:44 PM
*USIMZOEE KIASI CHA KUPOTEZA UHURU WAKO.*
Mahusiano yanapaswa kuwa na uwiano kati ya Upendo na Uhuru. Usimzoee mwanamke kupita kiasi hadi unashindwa kufanya maamuzi yako binafsi au unamhofia kupita kiasi.
*Mwanamke anayekupenda kweli atakuheshimu zaidi ukiwa na msimamo na maisha yako nje ya mahusiano.*
_Mapenzi si utumwa, wala hayatakiwi kukufanya ujisahau._ Usiruhusu hisia zako zikuongoze hadi ukajikuta unamfanya yeye kuwa kila kitu. *Mwanamume mwenye thamani yake hujitegemea kihisia na ana uwezo wa kuendelea na maisha hata bila uhusiano.*
Ikiwa huwezi kumuacha mwanamke kwa sababu umemzoea sana uwepo wake, basi tayari umepoteza udhibiti wa maisha yako. Mwanamke anapenda mwanaume anayejua thamani yake na anayesimamia maisha yake bila kuyumbishwa.
_*Linda uhuru wako, jithamini, na hakikisha heshima yako inabaki imara.*_
*Hapo ndipo utaheshimiwa na kupendwa kwa dhati.*
*ONYESHA THAMANI YAKO*
WhatsApp In-box ๐ https://wa.me/message/36OZ47M2H4RAA1
WhatsApp Channel OTHUMAN FACT Channel. ..https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s

๐
โค๏ธ
๐จ๐ฉ
๐
๐งโโ๏ธ
6