𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧 WhatsApp Channel

𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧

611 subscribers

About 𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧

> Unahitaji maarifa ya maisha, mahusiano, heshima na mafanikio ya kweli? Jiunge na OTHUMAN FACT, channel inayogusa hisia, akili na maisha halisi. Kila siku tunakuletea uhalisia, ukweli na ushauri unaoweza kukusaidia kubadilika na kusonga mbele. BONYEZA HAPA KUJIUNGA. ..https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s *-Mimi naitwa OTHUMAN FACT, ni mshauri wa maswala yote ya kijamii Mahusiano/Mapenzi, Ndoa, Saikolojia, Biashara, Afya. Pia utapata kuelewa namna sahihi ya kuyaishi Maisha yako n.k Ahsante.* _Sevu namba ya WhatsApp Tuma Majina yako Ili kupata masomo ya ziada STATUS Bonyeza Link_ ..https://wa.me/message/36OZ47M2H4RAA1 Tuma Majina yako In-box. *Instagram* https://instagram.com/othumanfact?igshid=ZGUzMzM3NWJiOQ== *Facebook* https://www.facebook.com/profile.php?id=100075802703307&mibextid=ZbWKwL *TikTok* https://www.tiktok.com/@othuman.fact?_r= *WhatsApp Channel* https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s

Similar Channels

Swipe to see more

Posts

𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/23/2025, 2:16:10 PM

Kupendwa kunajenga misingi ya: i/ Uaminifu ii/ Kujitolea iii/ Uvumilivu Kuhitajika kunapoteza mvuto wake pale ambapo unashindwa kutimiza kile ulichokuwa unatoa. Mapenzi ya kweli hayaegemei kile unachotoa, bali ni wewe kama mtu mzima mwenye thamani yako. Unajuae Kama Unapendwa Au Unahitajika Unatakiwa kujiuliza Je, mtu huyu yuko upande wangu hata nikishindwa? Je, anaonyesha kujali kuhusu hisia zangu au anajali anachopata kutoka kwangu? Je, akipata mtu mwingine bora kwangu kifedha, kimuonekano, atabaki au ataondoka? Katika dunia ya leo yenye misukosuko mingi ya maisha na mahitaji ya kila aina, ni rahisi kujikuta katika mahusiano ya KUHITAJIKA kuliko ya KUPENDWA. Lakini fahamu hivi. Kuhitajika ni mzigo, kupendwa ni baraka. Jenga mahusiano yanayotokana na moyo, si kutokana na maslahi ya mtu. Na wewe mwenyewe, jipime je, unapenda au unahitaji? Kwa wale wanaoamini maandiko. Kasomeni *(1 Wakorintho 13:4–8)* _"Upendo huvumilia, hufadhili, hauhusudu, haujivuni, haujitakasi, haukasiriki upesi, hauhesabu mabaya… Upendo hauishi_ **Quran kasome Surat Ar-Rum (30:21)* _"Na miongoni mwa Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao, naye ameweka baina yenu mawaddah (mapenzi) na rahmah (huruma). Hakika katika haya zimo Ishara kwa watu wanaofikiri."_ Maana yake nini pendo la kweli halitokani na maslahi, bali ni la *kiroho, kihisia na kiutu.* Upendo wa kweli unaendana na utulivu wa nafsi, heshima, na kujali sio tu kutimiza mahitaji bali kuonyesha huruma na uvumilivu. Follow na share kwa wengine 👉 [Othuman Fact Channel] (https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s)

❤️ 🫡 2
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/24/2025, 3:22:26 AM

💞 *MKE WAKO KIPENZI CHA MOYO WAKO.* 💞 > OTHUMAN FACT CHANNEL Katika Kitu Kidogo Mno na Chepesi Mno Kukiteka na Kukimiliki Kwa Mwanaume Mwenye Kujitambua ni Moyo na Upendo wa Mkewe. Sababu,,Hauhitaji Vikubwa wala Vyenye Gharama ili Ufurahi Bali Huhitaji Vidooogo Vyenye Thamani Ndani ya Moyo na Wala Havihusishi Gharama ya Mfukoni. Kwa MUME Ambae Haoni Kamwe Hatoiona Thamani na Wala Hatojali Kukithamini Kitakachomthaminisha Mke Wake. Wala Kushughulishwa na Vyenye Kumpa Furaha Mke Wake. 'Mkeo Tamaa yake Si Pesa,,,Bali Tamaa yake ni Thamani ya Moyo wake na Mapenzi yako juu yake. Na Ukimnyima Thamani yake Usishangae Akahamia Kwenye Pesa Zako,,Ambazo Umezipa Muda Mrefu Kuzitafuta Kuliko Kuitafuta Furaha Yake. Uthamini Moyo Wake,,Atakuthamini na Atavithamini Vyote vya Kwako wala Hatoviharibu wala Kuvisambaratisha. Mpe Upendo Mke Wako,,,Atakufunulia Ukurasa Wake wa Upendo Kwani Mke Wako Ana Upendo Mwingi wa Dhati na Ufunguo wa Ukurasa Huo wa Upendo wake ni Upendo wako. Mpende Atakupenda. Mpe Muda Wa Kuwa Na Wewe,, Nae Ataupa Muda Moyo wako na Mapenzi yako Katika Moyo wake,,,Na Ataupa Thamani yake Stahiqi Ukiumia Naye Ataumia,,Ukihuzunika naye Huhuzunika. Msikilize Mkeo Naye Hatoacha kukusikiliza Wala Kudharau Mazungumzo yako. Hata Ukihisi Wewe ndio Unaongea vya Maana Basi Jua Kama Humsikilizi Mkeo Hayo Maneno yako Kwake ni Pumba Tu Mke Hulipiza Tabia yako. Mfanye Kuwa Rafiki yako Cheza nae Taniana nae Furahi na Utafurahika USO wake na Kukinai Moyo wake na Kujaa Upendo wake juu YAKO na Huzidi Thamani yako Katika Moyo wake. Mahabbah_Yako. Ni Zawadi na Chakula cha Moyo wa Mkeo Mlishe Usimuache Njaa. Follow na share kwa wengine 👉 [Othuman Fact Channel] (https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s) Nawatakia ndoa yenye furaha...❤❤❤

❤️ 😭 3
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/25/2025, 5:13:58 AM
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/23/2025, 2:15:27 PM

Watu wengi wanaingia kwenye mahusiano wakiamini wanapendwa, kumbe wanahitajika tu. Kupendwa na kuhitajika ni maneno mawili ambayo mara nyingi huchanganywa, lakini kiuhalisia yana tofauti kubwa sana. Kupendwa ni mtu kukujali kwa dhati, kukuona wa thamani bila kuangalia faida yoyote anayopata kutoka kwako. Atakuheshimu hata mbele za watu. Atakuelewa hata katika mapungufu yako. Atachagua kukusamehe, hakukuacha. Atakutafuta hata ukiwa huna chochote cha kutoa. Tafiti za kisaikolojia zinaonyesha kuwa watu wanaohisi kupendwa kwa dhati hupata viwango vya juu vya utulivu wa kihisia na afya ya akili. Kuhitajika kunakuwa ni kwa sababu unatoa msaada, faraja, pesa, au hata kuondoa upweke kwa mtu (ngono). Wakati mwingine mtu anakuambia “nakupenda” kumbe maana yake ni: “Nakuhitaji kwa sasa.” Mtu anayekuhitaji: Anaweza kukuacha akipata mtu mwingine mwenye msaada zaidi yako. Anakuwa na upendo wa muda tu. Anapokuwa na mahitaji, anakukaribia sana; mahitaji yakitoweka, anakutoweka pia. Utafiti wa Harvard (2020) uligundua kwamba asilimia kubwa ya ndoa zinazovunjika ndani ya miaka mitano huwa zimejengwa juu ya "kuhitajiana" kuliko "kupendana kwa dhati". Follow na share kwa wengine 👉 [Othuman Fact Channel] (https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s) 👇👇👇👇👇👇👇

𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/24/2025, 12:58:58 PM

*Ukombozi wa kweli wa mwanamke hauko kwenye kuwa sawa na mwanaume,* ila upo kwenye kuwa bora zaidi katika nafasi yake ya kipekee kama Mwanamke. *Mwanamke akiishi kwenye asili yake, jamii itapona, ndoa zitadumu, na watoto watakua kwenye misingi ya haki, upendo na heshima vitadumu.* Mwanamke akirudi kwenye asili yake, familia itasimama, familia ikisimama, *taifa litastawi.* Follow na share kwa wengine 👉 [Othuman Fact Channel] (https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s)

Post image
❤️ 👍 3
Image
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/24/2025, 8:34:19 PM

*Katika haya maisha tunayoishi ili uwe na furaha na kila mmoja na usiudhi yeyote ingia kwa watu kipofu na utoke bubu* *Unyamaze kwa kila unacho ona kwani kuna mengine kuyasema kwake nikuamsha fitina iliyolala* *Na kisha epuka Sana kufichua siri za watu kwani haingii peponi mwenye. Kufichua siri za watu na kuvunja heshima za watu* *Nyamazia kila unachosikia Usiwe ni mwenye kugombanisha watu na ukishidwa kabisa nyamaza kwani kunyamaza ni hekma lakini ni wachache wanayoitenda* https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s

Post image
❤️ 🫡 2
Image
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/25/2025, 6:52:08 AM

*Katika mahusiano au Ndoa unahitaji sana Nguvu ya Mungu ili kudumu* Ukija huku na mtazamo wa kutaka kila kitu kila wakati kizunguke na kuegemea upande wako na matakwa yako tu, utaharibu jambo. Itakubidi ujitese mara kadhaa ili kuhakikisha uhusiano unampa nafasi na faraja mwenzi wako pia. Kuingia katika mahusiano au ndoa bila kuwa na uwezo wa kunyumbulika na kuwa tayari kujirekebisha ili mahitaji na asili ya mwenzi wako yapate nafasi ya kuonekana na kuridhika, ni sawa na kuiua hiyo ndoa/uhusiano kabla hata haijaanza. Kusema kwamba "Sipendi kutoka nje na siwezi kubadilika" haitafanya kazi mtu wangu. i/. Mimi sio wa kupiga simu sana" ii/. Mimi sio wa kuzungumza sana... iii/. Mimi sio... Mimi sio.. iv/. Ndivyo nilivyo tu, mimi... v/. Sio hivyo ninavyopenda.. Mchele au Maharage. Taa ziwe zimewashwa au zimezimwa. Dadeki *Katika uhusiano au ndoa, unalazimika kujifunza/kufundwa na kujitolea kupokea mambo mapya na tabia mpya, na pia kuachana na baadhi ya mambo na tabia zako za zamani Ili uendane na mahitaji ya ndoa.* Usije na fikra zilizoganda kama unataka uhusiano au ndoa yako iwe bora. Elewa, na jifunze, kunyumbulika. *WEWE SIO MNARA.* Follow na share kwa wengine 👉 [Othuman Fact Channel] (https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s)

Post image
👍 ❤️ 4
Image
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/25/2025, 6:27:36 AM

*Hakuna hekima ila ni upumbavu unaotokana na ujinga kwa mtu kujivisha mkanda mnene wa UNAFIKI na MAJIVUNO wakati wa uchumba na urafiki wa kimapenzi.* > OTHUMAN FACT CHANNEL *Unasimika msingi wa uongo katika maisha yako ya ndoa, unajifanya kuwa una kile ambacho kimsingi hauna kabla au wakati wa uchumba.* Hauwezi kuuficha Ukweli milele. Kuna mambo ambayo unaweza kuyaficha wakati wa uchumba, lakini ndoa itayafichua. *Sasa kwa nini ujisumbue?* Unakopa nguo, viatu, gari, hata nyumba ili tu kumvutia mtu. Unadanganya kuhusu jina lako, asili ya familia yako, kiwango chako cha elimu, mahali unapofanya kazi, eeh jamani, haumwogopi hata Mungu wako? *Unadanganya adi chakula unapenda kinabadilika ghafla kutoka maharagwe kwenda pizza.🤣* Mtu ambaye hujawahi hata kula pizza maishani mwako Leo unasema *"chakula changu pendwa ni pizza na hot dog",* ilhali unapenda furu na supu ya mboga, hot dog ikuchome mdomo huko, 😂 Mwingine utasikia anaanza kuongea Kiingereza cha kifalme, *"in it, in it"* 🤣🤣 Mwisho wa siku Lahaja ya Kimarekani inawaangukia ghafla kama vazi la Eliya *Wengine wanadanganya hata kuhusu hali zao za usichana/usafi (tazama huyo), na baadhi ya kidada wanaaki kabisa, makalio, mapaja, kama bajeti ya taifa ilivyopakiwa, na kuingia katika ndoa ya kupakiwa, itakayovunjika kwa namna ya kupakiwa hutoamini... Kilichovuta na kumfanya akupende sio uharisia, kafata big nyash anakuja kukutana na small nyash 🤣.* Kitu kimoja unatakiwa kujua kuhusu Uongo na unafiki huu wote, Vyote vina muda wake wa kuisha....(expiredate😭) Huwezi kudanganya milele, ukweli utakapofichuka, nini kitatokea? Ushajiuliza au ndo unajiandaa maisha yako yote yawe ni maisha ya udanganyifu, kila siku uwe ni wakutafuta Uongo mpya Ili Mahusiano yenu Yaendelee??? *Suluhisho bora hapa ni Kuhuwa halisi, na kuwa wewe mwenyewe.* Mtu anayekupenda atakupenda tu. Mungu alipanga hivyo kwamba vile vitu ambavyo unavionea aibu, ndivyo vinavyomvutia huyo msichana au mvulana kwako. *Hauhitaji Kuwa Mkamilifu Ili upendwe kikamilifu.* "Watu hawakupendi kwa sababu wewe ni mkamilifu, Wewe unakuwa mkamilifu kwa sababu wao wanakupenda." *Epuka tamaa ya kudanganya wakati wa uchumba, utakuwa unatoa taarifa za uongo kwa mtu anayekupenda, na hilo lazima liwe na madhara mwishowe...* Ndugu Yangu Mwanaume, Kama ni gari tu huna kwa sasa, kuna dada huko nje ambaye atakupenda na kuwa na wewe kwa furaha, usijaribu kujifanya kuwa usivyo. Dada Yangu, *Hata kwa hilo tumbo lako ambalo limegoma kuwa flat hata baada ya mazoezi mengi makali ya kupunguza mwili, bado kuna mwanaume atakayekupenda hivyo hivyo Ulivyo mpaka ushangae.* *MUWE NA JUMAPILI NJEMA* Follow na share kwa wengine 👉 [Othuman Fact Channel] (https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s)

Post image
❤️ 2
Image
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/24/2025, 8:33:47 PM

*MUDA WOTE AKILI YAKE IKO SAWA HAIJAVURUGWA, NA KILEVI🤣🤣🤣* Follow na share kwa wengine 👉 [Othuman Fact Channel] (https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s)

Video
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
𝗢𝗧𝗛𝗨𝗠𝗔𝗡 𝗙𝗔𝗖𝗧
5/24/2025, 7:39:11 AM

Channel name *OTHUMAN FACT* Link https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s *SAMBAZA MARA NYINGI UWEZAVYO*

Link copied to clipboard!