๐ข๐ง๐๐จ๐ ๐๐ก ๐๐๐๐ง
February 7, 2025 at 12:39 PM
*NINI KINATUFANYA TUWE BINADAMU?*
Jua lilikuwa linazama huku upepo mwanana ukivuma taratibu. *Nilikuwa nimekaa kwenye benchi la bustani moja hivi la Manisipaa ya Geita, nikitafakari maisha.* Ghafla, nilimuona mzee mmoja mwenye ndevu nyeupe, akiwa amevaa shati jeupe lilikuwa limechakaa kidogo haikuwa ishu.
Alikuwa amekaa pembeni yangu, akitazama watoto waliokuwa wakicheza mbali kidogo kutokea pale tulipokiwa sisi.
Baada ya muda, niligeuka na kumsalimia. *โShikamoo Mzee.โ*
Akajibu kwa sauti ya utulivu, *โMarahaba kijana. Unaonekana una mawazo kidogo.โ*
Nikacheka kidogo na kusema, _โNi kweli, mzee wangu. Nafikiria baadhi ya vitu kuhusu maisha.โ_
Akatingisha kichwa kisha akasema, *โUnajua, kijana wangu, maisha ni fumbo. Lakini kuna swali moja ambalo kila mtu anapaswa kujiuliza.โ*
Nikamuuliza, โSwali gani hilo, mzee wangu?โ
Akasema, *โNINI KINATUFANYA TUWE BINADAMU?โ*
Nilikaa kimya kwa sekunde chache, nikijaribu kutafakari jibu. Nikaamua kusema, โPengine ni akili zetu, uwezo wa kufikiria na kubuni baadhi ya mambo mapya.โ
Mzee akatikisa kichwa kumaanisha, *โHapana, wanyama pia wana akili zao. Ndege hujenga viota vya kushangaza, nyuki huunda mizinga kwa hesabu sahihi, na hata simba hujua kupanga mbinu za kuwinda.โ*
Nikajaribu tena, _โPengine ni lugha, zetu maana sisi tunawasiliana kwa maneno na maandishi?โ_
Mzee akatabasamu na kusema, *โHata wanyama wana lugha zao. Mbwa hubweka kutuonya, nyani wanawasiliana kwa ishara, na nyangumi huwasiliana kwa sauti zao za kipekee."*
Nikaanza kushindwa kupata jibu sahihi lipi, kisha nikamuuliza _, โKwa hiyo, nini kinatufanya tuwe binadamu?โ_
Mzee akavuta pumzi ndefu, kisha akasema, *โNi uwezo wa KUJALI.โ*
Nikamtazama kwa mshangao, _โUnamaanisha nini?โ_
Akasema kwa upole, *โBinadamu pekee ndiye anayejali hata asipokuwa na sababu ya moja kwa moja. Tunajali hata kuhusu watu tusiofahamu. Tunalia tukiona mateso ya wengine. Tunajitolea kusaidia pasipo kulazimishwa. Tunapenda, tunasamehe, na tunahangaika na mustakabali wa kizazi kijacho. Huu ndio Utu wetu.โ*
Nilikaa kimya nikitafakari maneno yake. Akaniangalia na kusema, _โKijana, usiwe na haraka ya maisha. Usisahau kujali, kupenda, na kusaidia wengine. Hapo ndipo utakapogundua maana halisi ya kuwa binadamu.โ_
Alisimama, akapiga hatua chache, kisha akageuka na kuniambia, *โUsisahau, kijana. Ubinadamu siyo kazi, ni wito.โ*
Alipotokomea, nilihisi kama vile nimepokea somo kubwa maishani mwangu Kwa kwenda tu maeneo yale.
*Kinachotufanya kuwa binadamu siyo akili, siyo lugha, siyo teknolojia, bali ni uwezo wetu wa kujali wengine hata kama hatunufaiki nao moja kwa moja.*
WhatsApp In-box ๐ https://wa.me/message/36OZ47M2H4RAA1
WhatsApp Channel OTHUMAN FACT Channel. ..https://whatsapp.com/channel/0029VaLtsI46buMBVNc8Q40s
๐
โค๏ธ
๐
๐ช
๐ค
9