SOKALOJIA
SOKALOJIA
January 31, 2025 at 04:04 AM
✍🏻 Sheria Namba Moja Ya Mpira Wa Miguu inazungumzia Eneo la Kuchezea, Yaani Uwanja. Hebu tujikumbushe kidogo kuhusiana na Sehemu kuu za Uwanja, Ulalo na Wima. ✍🏻 Kwa Ulalo (Horizontal), Uwanja wa mpira wa miguu unagawanyika katika sehemu tatu, ambazo ni: 1. Nusu Ya Kwanza (Defensive Third) – Golikipa na Walinzi hii ndo Sehemu yao ya kujidai. 2. Nusu Ya Pili (Middle Third) – Viungo Walinzi, Viungo Washambuliaji na Viungo Wa Pembeni, hapa ndio Sehemu huonyesha Ufundi wao. 3. Nusu Ya Tatu (Attacking Third) – Washambuliaji hutumia eneo hili kufumania Nyavu. ✍🏻 Kwa Wima (Vertical), Uwanja wa Mpira Wa Miguu Unagawanyika Katika Sehemu tano🤯, ambazo ni: 1. Winga Ya Kulia ( Right Wing/Flank) 2. Winga Ya Kushoto ( Left Wing/Flank) 3. Nusu Nafasi Ya Kulia ( Right Halfspace) 4. Nusu Nafasi Ya Kushoto (Left Halfspace) 5. Katikati (Centre). ✍🏻 Unakitu cha kufundisha kuhusiana na Soka?, Wasiliana Nami kupitia Simu No. 0760728723 (WhatsApp). #lielewesoka.
❤️ 🔥 3

Comments