Mr Chakushangaza Elimu Solutions
Mr Chakushangaza Elimu Solutions
February 7, 2025 at 12:31 PM
Mwongozo wa Kuandaa Ombi la Ajira katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Ikiwa unapanga kutuma maombi ya kazi katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ni muhimu kuhakikisha kuwa umeandaa nyaraka zote zinazohitajika kwa usahihi na kwa mpangilio mzuri. Hapa chini ni muhtasari wa mambo muhimu ya kuzingatia: 1. Wasifu Binafsi (Curriculum Vitae - CV) Andika CV iliyo rasmi na yenye mpangilio mzuri. Jumuisha majina ya referees watatu (3) pamoja na mawasiliano yao, ikiwa ni: Anuani ya posta Barua pepe (Email) Namba ya simu 2. Vyeti vya Kitaaluma Ni muhimu kuwasilisha nakala za vyeti vyako vya kitaaluma ambavyo vimethibitishwa (certified) na wakili au mamlaka husika. Vyeti hivyo vinapaswa kujumuisha: Cheti cha Chuo na Transcript Cheti cha Kidato cha Sita (Form 6) Cheti cha Kidato cha Nne (Form 4) Cheti cha Kuzaliwa Vyeti vya taaluma au utaalamu kutoka kwa bodi au mamlaka husika 3. Barua ya Maombi Iandikwe kwa Kiswahili au Kiingereza kwa lugha rasmi na yenye mpangilio mzuri. Ielekezwe kwa: KAMISHINA JENERALI (Commissioner General) Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) S.L.P 11491, Mchafukoge - Dar es Salaam Kwa kuandaa nyaraka hizi kwa uangalifu na kuhakikisha zinakidhi mahitaji yote, utaongeza nafasi yako ya kufanikiwa katika maombi yako ya kazi TRA. *KAMA HUNA CV njoo inbox nikuandalie CV kali sana kwa bei nafuu* By Mr Chakushangaza 0627368679

Comments