
Aviation Media Tanzania
February 7, 2025 at 01:55 AM
Ndege hiyo ilichukuliwa katika Jamhuri ya Dominika wakati wa ziara rasmi ya Rubio, ikiwa ni sehemu ya vikwazo vilivyowekwa na Marekani kwa utawala wa Venezuela.
Marco Rubio alisema;
"Kukamatwa kwa ndege hii ya Venezuela, iliyotumiwa kukwepa vikwazo vya Marekani na kutakatisha fedha, ni mfano wa nguvu wa azma yetu ya kuwajibisha utawala haramu wa Maduro kwa vitendo vyake haramu"
"Pamoja na Jamhuri ya Dominika na washirika wetu wa kikanda, tutaendelea kukabiliana na mpango wowote wa kukwepa vikwazo vya Marekani."
