DIRA LEO
DIRA LEO
January 31, 2025 at 05:44 AM
Mdau mwingine @Kipala yeye alikuwa na haya: Lugha ninayojua ni "akifanya hivyo atakiona cha mtemakuni". Ninaelewa ni kama tishio au onyo: akifanya kitu kisicho halali ataona matokeo yake yaani atapata adhabu. Mtemakuni (pia: mtema-kuni au mtema kuni) ni mtu anayepasua miti kuwa kuni. Kwa hiyo ana kazi nzitonzito pia ni watu wenye nguvu ya kimwili. Maana neno "kutema" hupatikana kwa maana mawili moja ni "kutema mate" mengine ni "kupasua kitu" kama ubao, miwa n.k. Sina uhakika juu ya asili ya usemi lakini nimeielewa hivyo: Hawa watemakuni ni watu wenye nguvu wanajua kuadhibu. Ukitaka kuiba kwao utaona jinsi gani wanavyoweza kujitetea. - au labda pia: Watemakuni ni watu wanaoishi katika mazingira magumu msituni wakifanya kazi hii nzito heri usijaribu kucheza nao...

Comments