DIRA LEO
DIRA LEO
January 31, 2025 at 05:44 AM
Mdau mwingine ni @Kwetunikwetu ambaye alisema: Mimi hili nilipata simulizi toka kwa jamaa mmoja wa Kenya ambae anasema kuna mwalimu aliwasimulia shule ya msingi juu ya kisa cha mtema kuni. Hiyo hadithi inasema hivi: Siku moja jamaa mtema (mkata) kuni alienda porini kukata kuni. Sasa akakuta mti mkubwa umeanguka na umekauka vizuri, ambao wenyeji wanaupenda sana kwa kutumia kwa vile kuni zake hazitoi moshi n.k. Sasa huyo mtema kuni akaanza kukata kuni na kurundika mzigo mkubwa tu. Jua lilipozidi kuwa kali jamaa akavua nguo akabaki uchi (hakutarajia mtu kutokea maeneo hayo kwa vile ni mbali na makazi ya watu) huku akiendelea na kupasua kuni toka kwenye lile gogo. Ikatokea jamaa akawa amechoka na pia jua kali, kwa hivyo akaamua kukaa juu ya lile gogo kupumzika. Sasa lile gogo lilikuwa lina ufa (kutokana na kutanuka kwa jua kali), kwa hivyo nyanya zikawa zimening'inia kwenye huo ufa. Baada ya kitambo kirefu kupita, jua nalo likawa linazama; kwa hivyo jamaa akaamua kunyanyuka ili ajitayarishe kuondoka. Sasa kumbe lile gogo lilikuwa limeshaanza ku-contract (kusinyaa); kwa hiyo nyanya zikashindwa kutoka. Jamaa wakati anakukuruka, huku contraction ya gogo inaendelea taratibu; jamaa akajikuta immediate options zimekauka kwa vile hakuweza kujinasua na shoka lilikuwa mbali hivyo hawezi kuzikata nyanya ili atoke. So, jamaa ndio akafia pale juu ya gogo baada ya mateso ya muda mrefu, kwani hata kelele alizopiga hazikuweza kusikika kijijini ambako palikuwa mbali. Kwa hivyo, ndugu, jamaa na marafiki walipomtafuta ndio wakamkuta jamaa amejifia juu ya gogo na nyanya zimenasa ndani ya gogo....! Kwa hivyo ikaonekana ni mateso makubwa mno mtu anayoweza kuyapata, so watu wakawa wanafanya reference kwamba ukifanya jambo baya/ukaidi n.k then utakiona cha mtema kuni
👍 1

Comments