DIRA LEO
DIRA LEO
January 31, 2025 at 05:45 AM
Mdau mwingine ni @Madam Koku: Mi huwa nafahamu simulizi tofauti kuhusu ''kukiona cha mtemakuni'', sikuwahi kusikia pia hizo zilipoelezwa hapo juu. Niliambiwa kuwa mtema kuni ni mtu anaekata kuni na alieenda kukata kuni porini na alipokuwa anataka kuzifunga kuni pamoja akawa anatafuta kamba, na bila kujua akamgusa nyoka akidhani ni kamba ili afungie kuni, loooo! kilichofuata ni mapambano... kwa hiyo hicho ndo kilikuwa ''cha mtemakuni'' nilichokifahamu. It is so intresting kuwa kuna simulizi tofauti tofauti kuhusiana na msemo uleule. Na nafikiri mambo kama haya yangehifadhiwa vizuri (yangekuwa well documented) ingesaidia kwa vizazi vijavyo hasa ukizingatia kiswahili kinakua sana sasa hivi ktk nch nyingi za Afrika.
👍 1

Comments