
DIRA LEO
January 31, 2025 at 05:46 AM
Mwisho tulimnukuu Mdau @Babuyao:
Mtemakuni hakika ni mpasuaji au mkataji wa kuni kama wengine walivyosema. Hadithi ya mkatakuni wengine wanasema wakati akikata kuni alikosea mahesabu (umakini)shoka likatua kwenye mguu likampasua na kumjeruhi sana. Kwa hiyo, kukiona cha mtemakuni ina maana ya kujiingiza kwenye shida ya kujitakia, ni kukosa umakini katika kutenda jambo ambapo baadaye mtu anakuja kujuta kutokana na shida atakayoipata. Kumbe, ni msemo wa onyo, wa kumtaka mtu awe mwangalifu ili mabaya yasimkute. Ni msemo unaotaka seriousness ya mtu katika kutenda ili kujiepusha na matokeo mabaya.