
Salafi Da'wah East Africa
February 1, 2025 at 05:46 PM
............
*هؤلاء هم الرجال*
*HAWA NDIO WANAUME.*
*🌼 _'Affan bin Muslim Abu Uthman as-Swaffar (Allah Amrehemu)._*
*_>>Alikusanya pamoja Ilmu na UchaMungu._*
_>>Swalih bin Ahmad bin Abdillah al-I'jliy amesema:_
_"Ametuhadithia baba yangu:_
*_"'Affan bin Muslim ni mtu wa Basrah, thiqah, thabt, mtu wa Sunnah._*
*Alipewa dinar elfu kumi ili asimuadilishe mtu fulani na wala asiseme-kuwa-:"Ni muadilifu wala-:sio muadilifu (katika Jarh na Taadil/Kujeruhi na Kuadilisha)."*
*Basi akakataa na akasema:*
*_"Wala sibatilishi haqi miongoni mwa haqi (nitabainisha hali yake kama ni muadilifu au sivyo)."_*
_>>Hanbal bin Ishaq amesema:_
Nimemsikia 'Affan akisema: *"Aliniita Ishaq bin Ibrahim (alikuwa amiri wa mji wao chini ya khalifa Ma-muun) basi akanisomea barua ambayo alimuandikia al-Ma-muun ( aliyekuwa khalifa) na ndani yake yake-kumeandikwa-:*
*_"Mtahini Affan (ili aseme kauli ya kufr na bida'h kuwa Quran imeumbwa) na muite ili aseme: "Qur'an ni kadhaa na kadhaa". Basi akisema hivyo mkubalie na mthibitishe juu ya jambo lake, na ikiwa hakukukubalia basi mkatie kile alichokuwa anapewa (kama mshahara/posho kutoka kwa mtawala)"_* na ilikuwa inamuendea yeye dirham mia tano kila mwezi.
Amesema 'Affan:
Basi akaniambia (yule Amiri): _"Unasemaje?"_
*Nikasoma:*
{قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ}
*_{{Sema: Yeye ni Allah Mmoja}}_* -(suratul-Ikhlas), hadi nikaihitimisha (sura hiyo).
*Kisha nikasema: _"Imeumbwa hii (yaani hawezekani)?!"_*
Basi akasema: _"Hakika Amirul-Mu'miniin anasema usipomuitikia (ukasema anavyotaka) anakata ulichokuwa unapewa (kama mshahara)."_
Basi nikasema;_*"Anasema Allah Taa'laa:*_
{وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُون}
*_{{Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.}}_*
*Basi akaninyamazia na nikajiondokea."*
(ص228 - كتاب صفة الصفوة - عفان بن مسلم أبو عثمان الصفار - المكتبة الشاملة)
*════ ❁✿❁ ════*
*Salafi Da'wah East Africa (Afrika Mashariki)*
❤️
3