Salafi Da'wah East Africa
February 24, 2025 at 03:34 AM
*YANAYOMFUNGUZA ALIYEFUNGA*
* لا يفطر الصائم إذا تناول شيئاً من المفطرات ناسياً أو جاهلاً أو مكرهاً، لقول الله تعالى: {رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذْنَا إِنْ نَسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا} [البقرة: ٢٨٦] .
وقوله: {إِلَّا مَنْ أُكْرِهَ وَقَلْبُهُ مُطْمَئِنٌّ} [النحل: ١٠٦] وقوله: {وَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ فِيمَا أَخْطَأْتُمْ بِهِ وَلَكِنْ مَا تَعَمَّدَتْ قُلُوبُكُمْ} [الأحزاب: ٥] .
▪Hafungui aliyefunga akifanya chochote kinachofunguza kwa kusahau au kwa kutojua au kwa kulazimishwa kwa nguvu; kwa kauli ya Allah Aliyetukuka [Tarjama] {Ewe Mola wetu usituadhibu tukisahau au tukikosea} [Al Baqarah:286]. Na kauli yake [Tarjama] {ila aliyelazimishwa kwa nguvu na moyo wake umetulia kwa imani} [An-Nahl:106]. Na kauli yake [Tarjama] { Na hamna juu yenu dhambi katika muliyokosea lakini katika yaliyokusudia nyoyo zenu} [Al Ahzaab:5].
* فإذا نسي الصائم فأكل أو شرب لم يفسد
صومه؛ لأنه ناس.
▪Basi akisahau aliyefunga, akala au akanywa, haiharibiki saum yake; kwa sababu amesahau.
* ولو أكل أو شرب يعتقد أن الشمس قد غربت أو أن الفجر لم يطلع لا يفسد صومه؛ لأنه جاهل.
▪Na lau atakula au kunywa akiitakidi kuwa jua limezama au kuwa alfajiri haijachomoza, haiharibiki saum yake; kwa sababu hakujua.
* ولو تمضمض فدخل الماء إلى حلقه بدون قصد، لم يفسد صومه؛ لأنه غير متعمد.
▪Na lau atasukutua, na maji yakaingia kooni mwake bila kukusudia, haiharibiki saum yake; kwa sababu hakukusudia.
* ولو احتلم في نومه، لم يفسد صومه؛ لأنه غير مختار.
▪Na lau ataota na kutokwa manii usingizini, saum yake haiharibiki; kwa sababu hana hiyari.
* المفطرات ثمانية وهي:
*Yanayofunguza ni mambo manane, nayo ni:*
أ- الجماع: وإذا وقع في نهار رمضان من صائم يجب عليه الصوم، فعليه مع القضاء كفارة مغلطة وهي عتق رقبة، فإن لم يجد فصيام شهرين متتابعين، فإن لم يستطع فإطعام ستين مسكيناً.
1.Tendo la ndoa: akilifanya anayelazimika kufunga katika mchana wa Ramadhani, basi atalazimika -pamoja na kuilipa hiyo siku-kafara kubwa; nayo ni kuacha mtumwa huru, asipopata, atafunga miezi miwili mfululizo, asipoweza, atalisha masikini sitini.
ب- إنزال المني يقظة باستمناء أو مباشرة أو تقبيل أو ضم أو نحو ذلك.
2.Kutoa manii ukiwa macho kwa punyeto (musterbation) au kugusa au kubusu au kukumbatia au mfano wake.
ج- الأكل أو الشرب سواء كان نافعاً أم ضاراً كالدخان.
3.Kula au kunywa sawa iwe na manufaa au madhara kama kuvuta sigara.
د- حقن الإبر المغذية التي يستغني بها عن الطعام؛ لأنها بمعنى الأكل والشرب. فأما الإبر التي لا تغذي فلا تفطر سواء استعملها في العضلات أم في الوريد، وسواء وجد طعمها في حلقه أم لم يجده.
4.Kudunga sindano lishe ambazo zinamtosheleza na chakula, kwa sababu ina maana ya kula na kunywa. Ama sindano ambazo si lishe hazifunguzi sawa azitumie katika misuli au katika mshipa, na sawa askie ladha yake kooni au asiskie.
هـ- حقن الدم مثل أن يحصل للصائم نزيف فيحقن به دم تعويضاً عما نزف منه.
وخروج دم الحيض والنفاس.
5.Kutia damu, kwa mfano; akitokwa damu aliyefunga, akatiwa damu kulipizia kilichomtoka.
6. Na kutokwa damu ya hedhi na nifaas.
ز- إخراج الدم بالحجامة ونحوها. فأما خروج الدم بنفسه كالرعاف أو خروجه بقلع سن أو نحوه فلا يفطر؛ لأنه ليس حجامة ولا بمعنى الحجامة.
7.Kutoa damu kwa Hijama na mfano wake. Ama damu kutoka yenyewe, kama kutokwa damu puani au kwa kutoa jino au mfano wake; hazifunguzi, kwa sababu si hijama wala haina maana ya hijama.
ح- القيء إن تقصده، فإن قاء بغير قصد لم يفطر.
8.Kutapika atakapokusudia, akitapika bila kukusudia hafungui.
📗[Nubadh fi swaiyam; cha Mwanachuoni ibn Utheymin -Allah amrehem]
════ ❁✿❁ ════
*Salafi Da'wah East Africa (Salafi Da'wah Afrika Mashariki)*
https://whatsapp.com/channel/0029VabMSx07tkj3R6Dou41f