Nurul Kitab Wa Sunnah
                                
                            
                            
                    
                                
                                
                                February 26, 2025 at 11:47 AM
                               
                            
                        
                            *❗❗NDUGU ZANGU TUMCHE ALLAAH ﷻ*
JAMBO LA TALAKA NI HALALI LAKINI LA MCHUKIZA ALLAAH ﷻ USIPENDE KUOA NA KUACHA 
*Wahurumieni Wanawake zenu Ndyo ALLAH ﷻ alicho tuhusia na Mtume ﷺ Kama Mwanaume Huna Huruma na Mke wako, Mtakua na Tofauti Gani❓❓Je,❓Hutambui kua Mkeo ni Dhaifu Wahitajia Kua na Kauli Njema Nasiyo kutoa talaka kama Vile Maji ya Kunywa, Jambo Hili la Chukiza Mnooo❗*
ALLAH ﷻ anasema
 وَعَاشِرُوهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ ۚ فَإِن كَرِهْتُمُوهُنَّ فَعَسَىٰ أَن تَكْرَهُوا شَيْئًا وَيَجْعَلَ اللَّهُ فِيهِ خَيْرًا كَثِيرًا
*Na kaeni nao kwa wema, na ikiwa mmewachukia, basi huenda mkakichukia kitu, na Allah ﷻ ametia kheri nyingi ndani yake.*
[Surah An-Nisa' 19]
Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema:
*katika Aayah nyingine ya sura hiyo hiyo Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anaendelea kututanabaisha*
وأخذن منكم ميثاقا غليظا
*“…Nao wanawake wamepokea kwenu ahadi thabiti (kuwa mtakaa nao kwa uzuri).”*
[An-Nisaa: 21]
*Mtume wetu Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  akielezea fadhila za tabia njema anasema:*
أكمل المؤمنين إيمانا أحسنهم خلقا, وخياركم خياركم لنسائهم خلقا
*❝Muumini aliyekamilika kwa imani ni yule mwenye tabia njema, na mbora wenu ni yule aliye mbora kwa wake zake kwa tabia.❞*
[Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
*Na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  amesema tena:*
خيركم خيركم لأهله , وأنا خيركم لأهلي
*❝Mbora wenu ni yule aliye mbora kwa mke wake, na mimi ni mbora kwa watu wangu wa nyumbani (ahli).❞*
[Ibn Maajah na Ad-Daarimy]
*Na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema:*
إنّ المرأة خلقت من ضلع وإنّ أعوج شيئ في الضّلع أعلاه , فإن ذهبت تقيمه كسرته , وإن تركته لم يزل أعوج , فاستوصوا بالنساء
 
*Mwanamke Ameumbwa kwa ubavu, na sehemu iliyopinda ya ubavu ni juu yake, ukijaribu kuunyoosha utauvunja, na lau utauacha utaendelea kupinda, nakuusieni (kuwafanyia wema) wake zenu.”*
[Al-Bukhaariy na Muslim]
*Tuishi kama alivyo tuelekeza Mtume ﷺ na ALLAH ﷻ Mwanaume watakikana uwe na Subra na Uvumilivu usiwe kama Mkeo Mwanamke ni Mdhaifu Sana*
*والله أعلم*
     ⚖════❁(🔘)❁════⚖
Mja dhalili kwa ALLAH ﷻ: *Abūl Qayyim al sa'adiyy-Allaah amhifadhi*
Kwa faida zaidi Tembelea Channel yetu kupitia kiunganishi👇
WhatsApp Channel 
https://whatsapp.com/channel/0029VaZ971X2kNFh1Yng9447
Jiunge na Telegram👇👇
https://t.me/+q05hwRmp4uNiYzJk
                        
                    
                    
                    
                    
                    
                                    
                                        
                                            ❤️
                                        
                                    
                                    
                                        3