ShombyInvestment
ShombyInvestment
February 25, 2025 at 02:59 PM
*β˜…π”πƒπŽππ†πŽ π–π„ππ˜π„ π‚π‡π”πŒπ•πˆ* β–ͺ︎Ardhi yenye chumvi nyingi ni tatizo kwa mimea kwa sababu inafanya mizizi ishindwe kunyonya maji vizuri. Hii inasababisha mimea kunyauka hata kama udongo una unyevunyevu. *β˜…πŒπ€πƒπ‡π€π‘π€ π˜π€ π”πƒπŽππ†πŽ π–π„ππ˜π„ π‚π‡π”πŒπ•πˆ πŠπ–π€ πŒπˆπŒπ„π€* *β–ͺ︎Mimea inashindwa kupata maji* Chumvi huvuta maji kutoka kwenye mizizi ya mimea, hivyo hata kama umemwagilia, mimea bado inaweza kunyauka na kukauka. *β–ͺ︎Virutubisho vya udongo vinaathirika* Udongo wenye chumvi huzuia mimea kupata virutubisho muhimu kama potasiamu na fosforasi. Badala yake, husababisha mkusanyiko wa sodiamu na kloridi ambazo zinaweza kuwa na sumu kwa mimea. *β–ͺ︎Dalili kwenye majani na mashina* β€’Majani hugeuka njano (kupoteza ukijani). β€’Ukingo wa majani unageuka kahawia na kukauka. β€’Mizizi na mashina yanaweza kuoza. *β–ͺ︎Ukuaji wa mimea unadhoofika* Mimea hukua polepole na kutoa mazao machache. Mazao kama mahindi, nyanya, na maharage huathirika zaidi. *β–ͺ︎Udongo unakuwa mgumu* Sodiamu nyingi hufanya udongo kushikana sana, hivyo maji na hewa haziwezi kupenya vizuri. Mizizi inashindwa kupata virutubisho vya kutosha *πŸͺ“πŸŒ±π“π”πŒπ€πˆππˆ π‹πˆπŠπŽ π’π‡π€πŒππ€ππˆ 🌾🚜* *πˆππ€π„ππƒπ„π‹π„π€*
πŸ‘ 🫑 2

Comments