
NURU YA UPENDO
May 24, 2025 at 08:54 AM
*TAFAKURI YA MCHANA:*
Bwana Yesu asifiwe...mwana wa Mungu.
Tukumbuke, Kuenenda kwa Roho (Wagalatia 5:25) ni kutembea katika *nia ya Kristo* na sio nia zetu.
Nia ya Kristo ni kujishughulisha na mambo ya wengine na unyenyekevu,
_Wafilipi 2:3-9_
_[3]Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake._
_[4]Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine._
_[5] *Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;*_
_[6]ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;_
_[7]bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;_
_[8]tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba._
_[9]Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;_
Tuamkapo tulalapo, tutembeapo, tusiipoteze nia hii ya Kristo.
Neema ya Kristo iwe nawe
Itendee kazi nia hiyo kwa kumwambia mwenye dhambi mmoja juu ya Kristo aokoaye, Utatenda vema.
Bwana akubariki.
*www.nuruyaupendo.com*
🙏
❤️
👍
💯
😢
👏
47