NURU YA UPENDO
NURU YA UPENDO
May 24, 2025 at 08:54 AM
*TAFAKURI YA MCHANA:* Bwana Yesu asifiwe...mwana wa Mungu. Tukumbuke, Kuenenda kwa Roho (Wagalatia 5:25) ni kutembea katika *nia ya Kristo* na sio nia zetu. Nia ya Kristo ni kujishughulisha na mambo ya wengine na unyenyekevu, _Wafilipi 2:3-9_ _[3]Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake._ _[4]Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine._ _[5] *Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;*_ _[6]ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;_ _[7]bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;_ _[8]tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba._ _[9]Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;_ Tuamkapo tulalapo, tutembeapo, tusiipoteze nia hii ya Kristo. Neema ya Kristo iwe nawe Itendee kazi nia hiyo kwa kumwambia mwenye dhambi mmoja juu ya Kristo aokoaye, Utatenda vema. Bwana akubariki. *www.nuruyaupendo.com*
🙏 ❤️ 👍 💯 😢 👏 47

Comments