Chama Imara Na Samia
May 19, 2025 at 04:42 PM
GAVU AONGOZA UJUMBE WA
TANZANIA KUTEMBELEA
MAKAO MAKUU YA HISENSE
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Idara ya Oganaizesheni, Ndg. Issa Gavu ameuongoza ujumbe wa Tanzania uliopo China, kutembelea makao makuu ya Kampuni ya uzalishaji vifaa vya kielektroniki ya Hisense yaliyopo katika mji wa Qindao, nchini humo.
Gavu na ujumbe wake huo kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamefanya ziara hiyo kiwandani hapo ikiwa moja ya shughuli zilizopo katika ratiba ya ziara hiyo.
ziara hiyo ni sehemu ya kuimarisha ushirikiano wa kihistoria kati ya Tanzania na China, pamoja na kudumisha uhusiano kati ya CCM na Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).
== ==