WIZARA YA MAMBO YA NJE

WIZARA YA MAMBO YA NJE

162.9K subscribers

Verified Channel
WIZARA YA MAMBO YA NJE
WIZARA YA MAMBO YA NJE
May 21, 2025 at 07:05 AM
Leo tarehe 20 Mei, 2025, Mhe. Cosato Chumi (Mb.), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italia nchini, Mhe. Giuseppe Coppola. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi za Wizara jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo hayo, Mhe. Balozi Coppola ameeleza kuhusu nia ya Serikali ya Italia kuendelea kuunga mkono jitihada za kuleta maendeleo zinazofanywa na Serikali chini ya uongozi mahiri wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika kuthibitisha hilo, Balozi Coppola amejulisha kuwa Italia iko katika hatua za mwisho za kukamilisha mkopo wa gharama nafuu wa Dola milioni 281 kusaidia utekelezaji wa Awamu ya nne ya Ujenzi wa Reli ya Kisasa. Vilevile, alijulisha kuhusu kurejeshwa kwa Tanzania katika orodha ya nchi zinazonufaika na mitaji inayowezesha kuboresha elimu ya ufundi stadi, ambapo kupitia mpango huo Tanzania itanufaika na ufadhili wa hadi Euro milioni 20. Katika hatua nyingine, Tanzania na Italia zilikubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano katika sekta ya uchumi wa buluu, uchukuzi na usafirishaji, mawasiliano na teknolojia ya habari, kilimo na ufugaji, ulinzi na usalama pamoja na biashara na uwekezaji.
😂 😢 2

Comments