
START TEK
June 3, 2025 at 02:56 PM
🚨 JE, UNAJUA JINSI AKAUNTI ZA WHATSAPP HUWA ZINAIBIWA?
Ukiwa hujajua, kuna mbinu hatari zinazotumiwa kuiba akaunti za WhatsApp – na mara nyingi huonekana ni kawaida, lakini zina madhara makubwa sana. Hebu tuangalie:
🔍 1️⃣. SIM SWAP SCAM
Mhalifu anapata taarifa zako (jina, namba ya simu, ID n.k.), kisha anaenda kwa kampuni ya simu kuomba SIM mpya akidai umezama au kupotea. Akifanikiwa:
📩 Atapokea SMS zako, ikiwemo WhatsApp verification code na kuiba akaunti yako.
🧠 2️⃣. SOCIAL ENGINEERING ATTACK
Hii ni mbinu ya kukudanganya utoe code ya WhatsApp:
❗ Unapokea SMS yenye 6-digit code
📞 Halafu unapigiwa simu au kuandikiwa DM ukidanganywa kuwa ni WhatsApp au kampuni fulani
😱 Ukitoa hiyo code – akaunti yako imekwenda!
🖥️ 3️⃣. WHATSAPP WEB HIJACK
Mtu akifikia simu yako kwa sekunde chache, anaweza ku-scan QR code kwa WhatsApp Web na akaanza kusoma chats zako zote bila wewe kujua.
🧪 4️⃣. MALWARE / LINKS ZA KUDANGANYA
Ukibofya link za ajabu kwenye SMS, WhatsApp au email – zinaweza kuingiza malware kwenye simu yako na kufungua njia kwa mhalifu kuiba taarifa zako.
✅ JINSI YA KUJILINDA:
🔐 Washa TWO-STEP VERIFICATION:
WhatsApp > Settings > Account > Two-step verification > Enable
❌ Usiwahi kumpa mtu code ya WhatsApp
⚠️ Epuka kubofya link usizozijua
👀 Thibitisha mara mbili mtu anayedai anatoka kampuni fulani
🔧 Unahitaji msaada kuwasha Two-step Verification au kukagua usalama wa WhatsApp yako?
👇 Tuma ujumbe sasa:
📷 Instagram: @prime_persuits
✉️ Email: [email protected]
Elimu ya kidigitali ni silaha bora dhidi ya uhalifu wa mtandaoni. Sambaza ili wengine wajifunze pia! 📲💡
—
#digitalsecurity #primepursuits #cyberawareness #internerbundle