SITTA SPORTS ARENA
                                
                            
                            
                    
                                
                                
                                June 9, 2025 at 12:08 PM
                               
                            
                        
                            *TERMINATOR AITWA TIMU YA TAIFA ⚽*
Kocha wa timu ya taifa ya Rwanda Amavubi, Adel Amrouche anasema ana mpango wa kumuongeza Kagere Meddie kwenye timu ya makocha ya timu ya taifa atakapostaafu soka.
Adel Amrouche amesema kuwa ni katika kupanua benchi la ufundi ambapo Kagere atakuwa mshauri na kocha wa washambulia kwenye timu ya taifa.
Meddie Kagere raia huyo wa Rwanda mwenye umri wa miaka 38 mzaliwa wa Uganda, amefanya vyema akiwa klabu ya Simba kabla ya kutimkia Singida Black Stars.
Mbali ya klabu ya Simba msakata kambumbu huyo alikipa katika timu za Kiyovu Sports ,Mukuru Victory ,Police FC,Rayon Sports,Gormahia Singida Fountain Gate na Namungo.
SITTA SPORTS UPDATES ⚽