
SITTA SPORTS ARENA
103 subscribers
About SITTA SPORTS ARENA
*Sitta Sports Arena ni chaneli ya michezo inayojihusisha na Habari mbalimbali za michezo, matokeo pamoja uchambuzi. Pata Habari za michezo kuanzia za ndani na zile za kimataifa.* *Sitta Sports Arena Deals with All Sports Updates and Sports analyst also Highlights of Football Match and results*
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

*KASONGO ASIMAMISHWA KAZI ⚽* Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amemsimamisha kazi Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania, Almas Kasongo. SITTA SPORTS UPDATES ⚽


*NDIMBO ATEMA CHECHE ⚽ 👇* "Klabu ya Yanga wamefika wameleta barua na kuondoka na wamesema hawana chochote cha kuzungumza, Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidao alimuita CEO wa Yanga wazungumze alikataa, hizi ni taasisi kubwa na sio kila jambo tunapaswa kuandikiana barua kama tunatoa posa"- Cliford Ndimbo. CHANZO: NasibuMkomwa. SITTA SPORTS UPDATES ⚽


*TRENT APEW JEZI YA MARCELO⚽👇* Trent Alexander-Arnold amejiunga rasmi na *Real Madrid* na kupewa jezi namba 12. Jezi hii ilikua ikivaliwa na mchezaji wa Timu ya Taifa ya Brazil Marcelo Viera ambae ameitumikia Klabu hiyo kwa mafanikio makubwa. Pichani anaonekana na rais wa klabu, Florentino Pérez, mbele ya makombe ya UEFA Champions League. Ujio wake unaimarisha safu ya beki wa kulia ya Madrid, akileta uzoefu mkubwa kutoka Liverpool. SITTA SPORTS UPDATES ⚽


*MADRID YATAMBULISHA UZI MPYA ⚽ 👇* *Huu hapa Uzi mpya wa Real Madrid* kwa msimu wa 2025/26. Inatengenezwa na *Adidas* na kudhaminiwa na *Emirates Fly Better*. Ubunifu wake una rangi ya asili nyeupe iliyo na mipira midogo ya kijivujivu kwa mbele, mistari ya bega myeupe na nyeusi, pamoja na mstari mwembamba wa dhahabu pembeni. Jezi hii inaonyesha mchanganyiko wa heshima kwa urithi wa klabu na muonekano wa kisasa unaoendana na mafanikio ya Real Madrid kitaifa na kimataifa. SITTA SPORTS UPDATES ⚽


*SIMBA WATOA TAARIFA HII KWA UMMA ⚽* Klabu ya Simba imesema itaingia uwanjani Juni 15, 2025 kwa ajili ya kushiriki mchezo namba 184 dhidi ya Yanga SC kama ilivyopangwa na Bodi ya Ligi Kuu. Aidha, imesema mabadiliko yoyote ya kujaribu kuahirisha mchezo huo ni batili na kinyume na taratibu za uendeshaji wa mpira wa miguu, na kwamba haitashiriki mchezo wowote wa namba 184 isipokuwa ule uliopangwa kuchezwa Jumapili. SITTA SPORTS UPDATES ⚽


*IBRAHIMOVIC AJA KUTALII TANZANIA ⚽* Nyota wa zamani wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic yupo Nchini Tanzania ambapo ame‘post’ picha akiwa eneo la Kogatende kwenye Hifadhi ya Taifa ya Serengeti nchini Tanzania eneo ambalo ni kitovu cha uhamaji wa wanyama maelfu wanaovuka Mto Mara. Zlatan (43) raia wa Sweden ambaye amewahi pia kuichezea Ajax, PSG, AC Milan na Barcelona ambaye kwa sasa ni sehemu ya washauri wa klabu ya AC Milan yupo Tanzania kwa ajili ya mapumziko ya mwisho ya msimu. SITTA SPORTS UPDATES ⚽


*UNITED WAMTANGAZA RASMI CUNHA ⚽👇* Matheus Cunha ametangazwa rasmi kuwa mchezaji mpya wa *Manchester United*. Akiwa anatokea Wolves, Cunha ni mshambuliaji wa Kibrazil anayejulikana kwa kasi, ubunifu na uwezo wa kucheza nafasi nyingi za mbele. Usajili huu unaipa Manchester United chaguo jipya safu ya ushambuliaji, na unaweza kumsaidia kuleta ushindani kwa Rasmus Højlund na kuongeza ubunifu katika eneo la mwisho la uwanja. Mashabiki wa United wanatarajia mchango wake utasaidia kuinua kiwango cha timu msimu ujao. SITTA SPORTS UPDATES ⚽


*MAGAZETI YA MICHEZO LEO TAREHE 13/JUNI/2025⚽👇* SITTA SPORTS UPDATES ⚽

*MAN UNITED WAZINDUA UZI MPYA ⚽ 👇* Hii ni jezi mpya ya *Manchester United* kwa msimu wa 2025/26, ikizinduliwa rasmi ndani ya *Old Trafford* mbele ya jukwaa la “Sir Alex Ferguson Stand”. Jezi ina muundo wa kisasa wenye mistari myekundu na nyeusi pembeni, ikiwa na *Snapdragon* kama mdhamini mkuu na *Adidas* kama mtengenezaji. Ubunifu wake unaleta hisia ya heshima kwa historia ya klabu huku ukionyesha mtazamo wa kisasa wa mafanikio. Mashabiki wengi wameipokea kwa hisia chanya. SITTA SPORTS UPDATES ⚽
