
JamiiForums
June 10, 2025 at 03:01 PM
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imesema imebaini uwepo wa vitendo vya Ukiukwaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa Sura 258 katika Mikutano ya Siasa, kwa baadhi ya Vyama kuruhusu Wanachama na mashabiki wake kutumia maneno ya Uongo, kashfa na uchochezi dhidi ya Chama kingine, Mtu binafsi, Taasisi au Serikali
Msajili amekiasa kila Chama cha Siasa chenye Usajili kamili, kuwaelimisha na kuwadhibiti Wanachama na Mashabiki wake, kuhakikisha hawakiuki Sheria za Nchi, hususani Sheria ya Vyama vya Siasa na Kanuni zake na inafuatilia mienendo ya Viongozi, Wanachama na Mashabiki wa Vyama vya Siasa
Soma https://jamii.app/MsajiliMaelekezo

😂
🚮
👍
🙏
❌
🗑️
😮
18